-
Mwisho Wenye Kutazamisha wa Dini ya Uwongo Waonekana KimbeleUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Babiloni Yashushwa Chini Kwenye Vumbi
3. Fafanua ukuu wa Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Babiloni.
3 Ebu lisikilize tangazo hili rasmi la kimungu linalosisimua: “Haya, shuka, keti mavumbini, ewe bikira, binti Babeli; keti chini pasipo kiti cha enzi, ewe binti wa Wakaldayo; maana hutaitwa tena mwororo, mpenda anasa.” (Isaya 47:1) Kwa miaka mingi, Babiloni amekalia kiti cha ufalme akiwa serikali kubwa ya ulimwengu yenye mamlaka. Amekuwa “utukufu wa falme”—kitovu chenye usitawi wa kidini, wa kibiashara na wa kijeshi. (Isaya 13:19) Babiloni anapofikia upeo, milki yake imetandaa hadi mbali kusini kwenye mpaka wa Misri. Kisha, anapomshinda Yerusalemu mwaka wa 607 K.W.K., inaonekana ni kama Mungu mwenyewe hawezi kumzuia kupata-pata ushindi! Basi, Babiloni anajiona kuwa ‘binti bikira,’ ambaye hataingiliwa kamwe na mvamizi wa kigeni.b
4. Babiloni atapatwa na nini?
4 Hata hivyo, “bikira” huyo kichwa kikubwa atadondoshwa kutoka kwenye kiti chake cha kifalme asiwe tena serikali kubwa ya ulimwengu isiyoweza kubishaniwa, ‘aketishwe mavumbini’ kwa kutiwa aibu. (Isaya 26:5) Hataonwa tena kuwa “mwororo, mpenda anasa,” mfano wa malkia wa kubembelezwa-bembelezwa. Hivyo basi, Yehova anaamuru hivi: “Twaa mawe ya kusagia, usage unga; vua utaji wako, ondoa mavazi yako [“rinda lako refu,” “NW”], funua mguu wako, pita katika mito ya maji.” (Isaya 47:2) Baada ya Babiloni kulitia utumwani taifa zima la Yuda, sasa yeye mwenyewe atatendwa kama mtumwa! Wamedi na Waajemi, wanaomwondoa katika kiti chake cha mamlaka, watamfanyisha kazi ngumu ya kumwaibisha.
-
-
Mwisho Wenye Kutazamisha wa Dini ya Uwongo Waonekana KimbeleUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
b Kwa Kiebrania, “bikira, binti Babeli” ni msemo unaomaanisha Babiloni au wakaaji wa Babiloni. Yeye ni “bikira” kwa sababu hakuna mshindi amewahi kumteka nyara tangu awe serikali kubwa ya ulimwengu.
-