-
Mwenyeji au Mgeni Mungu Akukaribisha!Mnara wa Mlinzi—1992 | Aprili 15
-
-
19. Kuhusiana na kurudi kwa Israeli, ni wonyesho gani wa kiunabii uliokuwako kwamba wageni wangehusika?
19 Bado, katika kutabiri kununuliwa tena na kurudi kwa watu wa Mungu, Isaya alitoa unabii huu wenye kushtusha: “Mataifa wataijilia nuru yako, na wafalme kuujia mwanga wa kuzuka kwako.” (Isaya 59:20; 60:3) Hilo lamaanisha zaidi ya kwamba wageni mmoja mmoja walikaribishwa, kwa kupatana na sala ya Sulemani. Isaya alikuwa akielekeza kwenye badiliko lisilo la kawaida katika cheo. “Mataifa” yangetumikia pamoja na wana wa Israeli: “Wageni [wasio wazalia, NW] watajenga kuta zako, na wafalme wao watakuhudumu; maana katika ghadhabu yangu nalikupiga, lakini katika upendeleo wangu nimekurehemu.”—Isaya 60:10.
-
-
Mwenyeji au Mgeni Mungu Akukaribisha!Mnara wa Mlinzi—1992 | Aprili 15
-
-
22. “Wageni” wamekujaje kufanya kazi pamoja na Waisraeli wa kiroho?
22 Vipi juu ya ‘wageni watakaojenga kuta zako’? Hilo pia limetukia katika wakati wetu. Mwito wa wale 144,000 ulipokuwa karibu kukamilika, umati mkubwa kutoka mataifa yote ulianza kumiminika kuabudu pamoja na Israeli wa kiroho. Hawa wapya zaidi wana lile tazamio lenye msingi wa Biblia la uhai wa milele kwenye paradiso ya kidunia. Ingawa mahali ambapo hatimaye watafanya utumishi wao mwaminifu pangekuwa tofauti, walifurahia kusaidia mabaki ya wapakwa-mafuta katika kuhubiri habari njema za Ufalme.—Mathayo 24:14.
23. “Wageni” wamesaidia wapakwa-mafuta kwa kadiri gani?
23 Leo, zaidi ya 4,000,000 ambao ni “wageni,” pamoja na wale mabaki ya wale ‘wenyeji wa mbinguni,’ wanathibitisha ujitoaji wao mbidiifu kwa Yehova. Wengi wao, wanaume kwa wanawake, vijana kwa wazee, wanatumikia katika huduma ya wakati wote wakiwa mapainia. Katika mengi ya yale makundi zaidi ya 66,000, wageni kama hao wanachukua madaraka wakiwa wazee na watumishi wa huduma. Mabaki hushangilia hilo, wakiona utimizo wa maneno ya Isaya: “Wageni watasimama na kulisha makundi yenu, na watu wa kabila nyingine watakuwa wakulima wenu, na watunzaji wa mizabibu yenu.”—Isaya 61:5.
-