-
Kutumikia Pamoja na MlinziMnara wa Mlinzi—2000 | Januari 1
-
-
6. Mlinzi katika unabii wa Yehova alitangaza habari gani njema, nayo ilitimizwa lini?
6 Dini isiyo ya kweli ilikuwa imepata ushindi ulioje! Hata hivyo, mamlaka ya Babiloni ilikuwa ya muda mfupi tu. Miaka ipatayo 200 kabla ya tukio hilo, Yehova aliamuru hivi: “Enenda, weka mlinzi; aonayo na ayatangaze.” Mlinzi huyo alikuwa na habari gani za kutangaza? “Babeli umeanguka, umeanguka; na sanamu zote za miungu yake zimevunjwa chini.” (Isaya 21:6, 9) Kwa hiyo, mwaka wa 539 K.W.K., tangazo hilo la unabii likatimia. Babiloni lenye nguvu lilianguka, na punde si punde watu wa agano wa Mungu wakarudi nchini kwao.
-
-
Kutumikia Pamoja na MlinziMnara wa Mlinzi—2000 | Januari 1
-
-
13. (a) Mlinzi wa Yehova ametangaza ujumbe gani? (b) Inaweza kusemwaje kwamba Babiloni Mkubwa ameanguka?
13 Mlinzi huyo aliona nini? Mara nyingine tena, mlinzi wa Yehova, jamii yake ya shahidi, alitangaza hivi: “Babeli umeanguka, umeanguka; na sanamu zote za miungu yake [Yehova amezivunja] chini”! (Isaya 21:9) Mara hii, baada ya Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, ni Babiloni Mkubwa, milki ya ulimwengu ya dini isiyo ya kweli, anayenyang’anywa mamlaka yake. (Yeremia 50:1-3; Ufunuo 14:8) Si ajabu! Vita Kubwa, kama ilivyojulikana wakati huo, ilianzia katika Jumuiya ya Wakristo, ambako makasisi wa pande zote walichochea mapigano kwa kuwatia moyo vijana wao wenye nguvu waende vitani. Ni aibu iliyoje! Mwaka wa 1919, Babiloni Mkubwa hangeweza kuwazuia Wanafunzi wa Biblia, kama vile Mashahidi wa Yehova walivyojulikana wakati huo, wasitoke katika hali yao ya kutotenda na kuanza kampeni ya kutoa ushahidi ulimwenguni kote ambayo bado yaendelea. (Mathayo 24:14) Jambo hilo likawa ishara ya kuanguka kwa Babiloni Mkubwa, kama vile tu kuachiliwa kwa Israeli katika karne ya sita K.W.K. kulivyokuwa ishara ya kuanguka kwa Babiloni la kale.
-