-
“Sasa Ninyi Ni Watu wa Mungu”Mnara wa Mlinzi—2014 | Novemba 15
-
-
17, 18. (a) Yehova atawapa watu wake maagizo gani Gogu atakapowashambulia? (b) Ni lazima tufanye nini ili Yehova atulinde?
17 Gogu atakapoanza kushambulia, Yehova atawaambia hivi watumishi wake: “Nendeni, watu wangu, ingia katika vyumba vyako vya ndani, na ufunge milango nyuma yako. Jifiche kwa kitambo kidogo mpaka hukumu itakapopita.” (Isa. 26:20) Wakati huo, Yehova atatupatia maagizo yatakayookoa uhai wetu, na huenda ‘vyumba vya ndani’ vikahusianishwa na makutaniko yetu.
18 Hivyo basi, ikiwa tunataka Yehova atulinde wakati wa dhiki kuu, ni lazima tutambue kwamba ana watu wake duniani waliopangwa katika makutaniko. Ni lazima tuendelee kushikamana nao na kuendelea kushirikiana kwa ukaribu na kutaniko letu. Acheni tujiunge na mtunga-zaburi kutangaza hivi kwa moyo wetu wote: “Wokovu ni wa Yehova. Baraka yako iko juu ya watu wako.”—Zab. 3:8.
-