-
Endelea Kuonya Juu ya Kazi ya Ajabu ya YehovaMnara wa Mlinzi—1991 | Juni 1
-
-
17, 18. Yehova amekuwaje taji ya fahari na ua la uzuri kwa watu wake?
17 Nabii Isaya hueleza hali yenye furaha ya wale ambao huchukua msimamo wao kwa ajili ya ibada safi. Asema hivi: “Katika siku ile BWANA [Yehova, NW] wa majeshi atakuwa ni taji ya fahari, na kilemba cha uzuri, kwa mabaki ya watu wake. Naye atakuwa roho ya hukumu kwake yeye aketiye ili ahukumu; naye atakuwa nguvu kwao wageuzao nyuma vita langoni.”—Isaya 28:5, 6.
-
-
Endelea Kuonya Juu ya Kazi ya Ajabu ya YehovaMnara wa Mlinzi—1991 | Juni 1
-
-
19. Ni nani aketiye ili ahukumu, na Yehova amekuwaje roho ya hukumu kwake?
19 Kwa Yesu, “yeye aketiye ili ahukumu,” Yehova amekuwa “roho ya hukumu.” Yesu alipokuwa duniani, alikataa kushindwa na roho yenye kulevya ya mapatano ya ulimwengu. Leo, akiwa Mfalme wa Yehova aliyetawazwa, anajawa na roho takatifu, na hiyo humwelekeza katika kufanya maamuzi yaliyosawazika, yenye kuona wazi. Katika Yesu, unabii huu umetimizwa: “Na juu yake roho ya Yehova itatulia, roho ya hekima na ya uelewevu, roho ya ushauri na uweza, roho ya maarifa na ya hofu kwa Yehova.” (Isaya 11:2, NW) Kweli kweli, kupitia Yesu, Yehova ‘atafanya hukumu kuwa ndiyo kanuni, na haki kuwa ndiyo timazi.’ (Isaya 28:17) Hali maadui waliolewa kiroho wakizidiwa katika uharibifu, haki itafanywa kwa jina takatifu la Yehova na kwa enzi kuu yake ya ulimwengu wote mzima.
-