Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Uwe Mwenye Furaha Unapomngojea Yehova kwa Subira
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2024 | Februari
    • KWA NINI YEHOVA ANATARAJIA TUNGOJE?

      Biblia inasema hivi: “Yehova anangoja kwa subira ili kuwaonyesha kibali, naye atainuka ili kuwaonyesha rehema. Kwa maana Yehova ni Mungu wa haki. Wenye furaha ni wote wanaoendelea kumtarajia.” (Isa. 30:18) Mwanzoni maneno hayo ya Isaya yalikusudiwa kwa ajili ya Wayahudi waliokuwa wakaidi. (Isa. 30:1) Lakini baadhi ya Wayahudi walikuwa waaminifu, na maneno hayo yaliwapa tumaini. Maneno hayo yanawapatia tumaini pia watumishi waaminifu wa Yehova leo.

      Hivyo, ni lazima tungoje kwa subira kwa sababu Yehova anangoja kwa subira. Ana wakati uliowekwa ambapo atakomesha mfumo huu, na anangojea hadi siku na saa hiyo ifike. (Mt. 24:36) Wakati huo, itakuwa wazi kabisa kwamba mashtaka ya Ibilisi dhidi ya Yehova na wale wanaomtumikia ni ya uwongo. Kisha, Yehova atamwondoa Shetani na wote wanaomuunga mkono, lakini ‘atatuonyesha sisi rehema.’

      Tunapoendelea kungoja, huenda Yehova asiondoe majaribu yetu, lakini anatuhakikishia kwamba tunaweza kuwa na furaha tunapomngojea. Kama Isaya alivyosema, tunaweza kuwa wenye furaha tunaposubiri kwa hamu au kutarajia jambo fulani zuri litukie. (Isa. 30:18)a Tunawezaje kuipata furaha hiyo? Mambo manne yanaweza kutusaidia.

  • Uwe Mwenye Furaha Unapomngojea Yehova kwa Subira
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2024 | Februari
    • a Neno la lugha ya awali lililotafsiriwa kuwa “wanaoendelea kumtarajia” pia linaweza kumaanisha “kutumaini au kutamani jambo fulani litukie,” hilo linaonyesha kwamba ni jambo la kawaida kutamani Yehova atukomboe.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki