-
Jinsi Yehova Anavyotusaidia Kuvumilia kwa ShangweMnara wa Mlinzi (Funzo)—2022 | Novemba
-
-
YEHOVA HUTUONGOZA
8. Maneno ya Isaya 30:20, 21, yalitimizwaje nyakati za kale?
8 Soma Isaya 30:20, 21. Jeshi la Babiloni lilipolizingira Yerusalemu kwa mwaka mmoja na nusu, watu walipata taabu hivi kwamba wakaizoea kama mkate na maji. Lakini kulingana na mstari wa 20 na 21, Yehova aliwaahidi Wayahudi kwamba ikiwa wangetubu na kubadili tabia yao, angewakomboa. Akimrejelea Yehova kuwa ‘Mfundishaji wao Mkuu,’ Isaya aliwaahidi watu hao kwamba Yehova angewafundisha jinsi ya kumwabudu kwa njia inayokubalika. Maneno hayo yalitimizwa Wayahudi walipowekwa huru kutoka utekwani. Yehova alithibitika kuwa Mfundishaji wao Mkuu, na kwa kufuata mwongozo wake, watu wake walifanikiwa kurudisha ibada safi. Leo, tumebarikiwa kwa sababu Yehova ndiye Mfundishaji wetu Mkuu.
-
-
Jinsi Yehova Anavyotusaidia Kuvumilia kwa ShangweMnara wa Mlinzi (Funzo)—2022 | Novemba
-
-
10. Ni katika njia gani tunasikia “neno nyuma [yetu]”?
10 Isaya anataja njia ya pili ambayo Yehova anatufundisha anaposema hivi: “Masikio yako mwenyewe yatasikia neno nyuma yako.” Hapa nabii huyo anamfafanua Yehova kama mfundishaji aliye makini ambaye anatembea nyuma ya wanafunzi wake, akiwaelekeza kwenye njia wanayopaswa kwenda na kuwapa mwongozo. Leo, tunasikia sauti ya Mungu nyuma yetu. Jinsi gani? Maneno ya Mungu yaliyoongozwa na roho yaliandikwa katika Biblia zamani sana, wakati ambao uko nyuma yetu kwa mbali sana. Basi, tunaposoma Biblia, ni kana kwamba tunasikia sauti ya Mungu kutoka nyuma yetu.—Isa. 51:4.
11. Ili kuvumilia kwa shangwe, tunahitaji kuchukua hatua gani, na kwa nini?
11 Tunawezaje kunufaika kikamili kutokana na mwongozo ambao Yehova anatupatia kupitia tengenezo lake na Neno lake? Ona kwamba Isaya alitaja mambo mawili. Kwanza, “hii ndiyo njia.” Pili, “tembeeni ndani yake.” (Isa. 30:21) Haitoshi tu kujua “njia.” Tunapaswa pia ‘kutembea ndani yake.’ Kupitia Neno la Yehova, kama linavyofafanuliwa na tengenezo lake, tunajifunza mambo ambayo Yehova anataka tufanye. Pia, tunajifunza jinsi ya kutumia mambo tunayofundishwa. Ili tuvumilie kwa shangwe katika utumishi wetu kwa Yehova, tunahitaji kuchukua hatua hizo mbili. Ikiwa tutafanya hivyo, tunaweza kuwa na uhakika kwamba tutapata baraka za Yehova.
-