Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Sasa Mwisho Umekufikia”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 8. (a) Igizo la Ezekieli lilikuwa na ujumbe gani wa tumaini? (b) Unabii kuhusu “nywele chache” ulitimiaje?

      8 Hata hivyo, Ezekieli alipotoa unabii kwa kuigiza, alitoa pia ujumbe wa tumaini. Kuhusu nywele ambazo Ezekieli alinyoa, Yehova alimwambia nabii huyo: “Utachukua nywele chache na kuzifunga katika pindo za vazi lako.” (Eze. 5:3) Amri hiyo ilionyesha kwamba Wayahudi wachache ambao wangetawanyika kati ya mataifa wangeokolewa. Baadhi ya “nywele [hizo] chache” zingekuwa kati ya wahamishwa ambao walirudi Yerusalemu baada ya kipindi kirefu cha miaka 70 utekwani Babiloni. (Eze. 6:8, 9; 11:17) Je, maneno hayo ya kinabii yalitimia? Ndiyo. Miaka mingi baada ya utekwa wa Wababiloni kwisha, nabii Hagai aliandika kwamba baadhi ya Wayahudi waliokuwa wametawanyika kwa kweli walirudi Yerusalemu. Walikuwa “wazee ambao walikuwa wameona ile nyumba ya kwanza,” yaani, hekalu la Sulemani. (Ezra 3:12; Hag. 2:1-3) Yehova alihakikisha kwamba ibada safi iliendelezwa kama tu alivyokuwa ameahidi. Sura ya 9 ya kitabu hiki, itazungumzia habari zaidi kuhusu kurudishwa huko.—Eze. 11:17-20.

  • “Nyoa Kichwa Chako na Ndevu Zako”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
      • Ezekieli afunga baadhi ya nywele zake kwenye upindo wa vazi lake.

        ‘Funga’

        Baadhi ya wahamishwa wangerudi Yerusalemu, na ibada safi ingerudishwa

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki