-
“Uyatie Alama Mapaji ya Nyuso”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
16. Je, tukiwa watu wa Yehova tunawatia alama wale watakaookoka? Eleza.
16 Watu wa Yehova hawawatii alama wale watakaookoka. Kumbuka kwamba Ezekieli hakuagizwa apite katikati ya Yerusalemu na kuwatia alama watu ambao wangeokoka. Vivyo hivyo, leo watu wa Yehova hawajaagizwa wawatie alama watu wanaostahili kuokoka. Badala yake, tukiwa watumishi katika nyumba ya kiroho ya Kristo, tumeagizwa tuhubiri. Tunaonyesha kwamba tunachukua kazi hiyo kwa uzito kwa kuhubiri kwa bidii kuhusu Ufalme wa Mungu na kutangaza kwa bidii onyo kwamba mwisho wa ulimwengu huu mwovu uko karibu sana. (Mt. 24:14; 28:18-20) Kwa hiyo, tunashiriki kuwasaidia watu wanyoofu wajiunge na ibada safi.—1 Tim. 4:16.
17. Watu wanahitaji kufanya nini sasa ili wakati ujao wastahili kutiwa alama ya kuokoka?
17 Ili watu waokoke uharibifu unaokuja, wanapaswa kuonyesha imani sasa. Kama tulivyoona, wale waliookoka Yerusalemu lilipoharibiwa mwaka wa 607 K.W.K. walionyesha kabla ya uharibifu kwamba walichukia uovu na kwamba waliipenda ibada safi. Ndivyo ilivyo leo. Kabla ya mwisho kuja, watu wanahitaji kulia “kwa uchungu na kwa maumivu makali”—kuhuzunika sana—kwa sababu ya uovu ulio ulimwenguni. Badala ya kuficha hisia zao, wanapaswa kuonyesha kwa maneno na matendo kwamba wanaipenda ibada safi. Wanawezaje kufanya hivyo? Wanapaswa kusikiliza habari njema inayohubiriwa leo, waendelee kuvaa utu kama wa Kristo, wabatizwe ili kuonyesha kwamba wamejiweka wakfu kwa Yehova, na kuwaunga mkono kwa ushikamanifu ndugu za Kristo. (Eze. 9:4; Mt. 25:34-40; Efe. 4:22-24; 1 Pet. 3:21) Wale tu wanaofanya mambo hayo sasa—na ambao wataingia katika dhiki kuu wakiwa katika ibada safi—ndio watakaotiwa alama ya kuokoka.
18. (a) Yesu atawatia lini alama watu wanaostahili na atafanya hivyo jinsi gani? (b) Je, watiwa mafuta waaminifu wanahitaji kutiwa alama? Eleza.
18 Kutiwa alama kwa wale wanaostahili kutafanyiwa mbinguni. Katika siku za Ezekieli, malaika walikuwa na jukumu la kuwatia alama watu waaminifu ili waokoke. Katika utimizo wa siku zetu, mwanamume aliye na kidau cha wino cha mwandishi anawakilisha Yesu Kristo “atakapokuja katika utukufu wake” akiwa Hakimu wa mataifa yote. (Mt. 25:31-33) Yesu atakuja wakati wa dhiki kuu, baada ya dini ya uwongo kuharibiwa.c Katika kipindi hicho muhimu, kabla tu ya Har–Magedoni kuanza, Yesu atawahukumu watu kuwa kondoo au mbuzi. Washiriki wa “umati mkubwa” watahukumiwa, au kutiwa alama, ili kuonyesha kwamba wao ni kondoo, na basi “watapata uzima wa milele.” (Ufu. 7:9-14; Mt. 25:34-40, 46) Namna gani watiwa mafuta waaminifu? Hawahitaji kutiwa alama ya kuokoka Har–Magedoni. Badala yake, watatiwa muhuri wa mwisho kabla ya kufa au kabla ya dhiki kuu kuanza. Kisha, wakati fulani kabla ya Har–Magedoni kuanza, watainuliwa kwenda mbinguni.—Ufu. 7:1-3.
-
-
Kulia kwa Uchungu na kwa Maumivu Makali, Kutiwa Alama, Kuponda—Lini na Jinsi Gani?Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
‘Kutiwa alama’
LINI: Wakati wa dhiki kuu
JINSI GANI: Mwanamume mwenye kidau cha wino cha mwandishi anawakilisha Yesu Kristo atakapokuja akiwa Hakimu wa mataifa yote. Washiriki wa umati mkubwa watahukumiwa kuwa wenye haki, au watatiwa alama kuwa kondoo, hivyo kuonyesha kwamba wataokoka Har–Magedoni
-