Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Uyatie Alama Mapaji ya Nyuso”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 7, 8. Wanaume waliokuwa na silaha za kuponda wangefanyaje kazi yao, na matokeo yalikuwaje?

      7 Basi, wale wanaume sita wenye silaha za kuponda wangetimizaje kazi yao? Ezekieli alisikia maagizo ambayo Yehova aliwapa: Mfuateni mwanamume mwenye kidau cha wino na muue kila mtu isipokuwa mtu yeyote aliye na alama kwenye paji la uso. Yehova aliwaagiza hivi: “Mnapaswa kuanzia mahali pangu patakatifu.” (Eze. 9:6) Watekelezaji hao wa hukumu walipaswa kuanzia katikati ya Yerusalemu, katika hekalu, ambalo halikuwa tena takatifu mbele za Yehova. Kwanza, walipaswa kuwaua “wazee waliokuwa mbele ya ile nyumba”—wale wazee 70 wa Israeli waliokuwa hekaluni wakiifukizia uvumba miungu ya uwongo.—Eze. 8:11, 12; 9:6.

  • “Uyatie Alama Mapaji ya Nyuso”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 9, 10. Taja baadhi ya watu waliookoka uharibifu wa Yerusalemu, na tunaweza kusema nini kuwahusu?

      9 Soma 2 Mambo ya Nyakati 36:17-20. Unabii wa Ezekieli ulitimizwa mwaka wa 607 K.W.K. jeshi la Babiloni lilipoharibu Yerusalemu na hekalu lake. Wababiloni walikuwa kama ‘kikombe mkononi mwa Yehova,’ ambacho alikitumia kumwaga adhabu juu ya jiji la Yerusalemu lililokosa uaminifu. (Yer. 51:7) Je, kila mtu aliuawa? Hapana. Maono ya Ezekieli yalikuwa yametabiri kwamba baadhi ya watu hawangeuawa na Wababiloni.—Mwa. 18:22-33; 2 Pet. 2:9.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki