Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Unabii Kumhusu Masihi​—Mwerezi Mkubwa
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
      • Chipukizi changa la mwerezi lililopandwa juu ya mlima.

        4. Yehova amweka Mwana wake juu ya Mlima Sayuni ulio mbinguni

  • “Nitamweka Mchungaji Mmoja”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 9 Unabii huo unasema nini? (Soma Ezekieli 17:22-24.) Sasa Yehova ndiye atakayechukua hatua bali si tai wakubwa. Atachukua chipukizi changa “kutoka katika kilele cha mwerezi mkubwa na kulipanda . . . juu ya mlima mrefu na ulio juu sana.” Chipukizi hilo litasitawi na kuwa “mwerezi mkubwa” na kuandaa makao kwa ajili ya “ndege wa kila aina.” Kisha “miti yote ya shambani” itajua kwamba Yehova ndiye aliyeufanya mti huo mkubwa usitawi.

      10 Jinsi unabii huo unavyotimizwa. Yehova alimchukua mwana wake, Yesu Kristo kutoka kwenye ukoo wa kifalme wa Daudi (“mwerezi mkubwa”) na kumpanda juu ya Mlima Sayuni ulio mbinguni (“mlima mrefu na ulio juu sana”). (Zab. 2:6; Yer. 23:5; Ufu. 14:1) Kwa hiyo, Yehova alimchukua Mwana wake, ambaye alionwa na adui zake kuwa “mwanadamu wa hali ya chini zaidi” na kumkweza kwa kumpa “kiti cha ufalme cha Daudi baba yake.” (Dan. 4:17; Luka 1:32, 33) Kama mwerezi mkubwa, Mfalme wa Kimasihi Yesu Kristo atatawala dunia nzima na kuwaletea raia zake wote baraka. Kwa kweli, huyo ndiye Mtawala tunayepaswa kumtegemea. Chini ya kivuli cha utawala wa Ufalme wa Yesu, wanadamu waaminifu duniani kote ‘wataishi kwa usalama bila kuhangaishwa na woga wa msiba.’—Met. 1:33.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki