Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mtakuwa Hai”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • “Mifupa Ikaanza Kukaribiana”

      10. (a) Andiko la Ezekieli 37:7, 8 lilitabiri jambo gani kuhusu watu wa Mungu? (b) Ni mambo gani ambayo yaliwasaidia hatua kwa hatua watu wanaomwogopa Mungu waliokuwa uhamishoni wawe na imani?

      10 Nyakati za kale, Yehova alitabiri kwamba watu wake wangefanywa tena kuwa hai hatua kwa hatua. (Eze. 37:7, 8) Basi ni mambo gani ambayo yaliwafanya watu wanaomwogopa Mungu waliokuwa uhamishoni wawe na imani kwamba tumaini lao la kurudi Israeli lingetimizwa? Chanzo kimoja cha tumaini kilikuwa maneno ya unabii yaliyosemwa zamani na manabii. Kwa mfano, Isaya alikuwa ametabiri kwamba watu waliobaki, “mbegu takatifu,” wangerudi katika nchi yao. (Isa. 6:13; Ayu. 14:7-9) Pia, unabii mwingi kuhusu kurudishwa ambao Ezekieli alikuwa ameandika bila shaka uliendelea kuwapa tumaini. Isitoshe, kuwepo kwa wanaume waaminifu kama vile nabii Danieli huko Babiloni—na pia kuanguka kwa jiji la Babiloni mwaka wa 539 K.W.K.—kuliimarisha tumaini la wahamishwa kwamba wangerudi.

      Mkusanyo wa Picha: 1. Charles T. Russell akisoma Biblia. 2. Charles T. Russell na wenzake.

      SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 10A: Ibada Safi​—Yarudishwa Hatua kwa Hatua

      11, 12. (a) “Israeli wa Mungu” walirudishwaje hatua kwa hatua? (Tazama pia sanduku “Ibada Safi—Yarudishwa Hatua kwa Hatua.”) (b) Maneno ya Ezekieli 37:10 yanatokeza swali gani?

      11 “Israeli wa Mungu,” yaani, kutaniko la Wakristo waliotiwa mafuta walirudishwaje hatua kwa hatua kwa njia kama hiyo? Kwa karne nyingi, wakiwa katika hali ya utekwa ulio kama kifo, “sauti ya vitu vinavyogongana,” ilisikika watu wanaomwogopa Mungu walipotetea ibada ya kweli. Kwa mfano, katika karne ya 16, William Tyndale alitafsiri Biblia katika Kiingereza. Makasisi wa kanisa Katoliki walikasirika kwa sababu hawakutaka Biblia isomwe na watu wa kawaida. Tyndale aliuawa. Hata hivyo, watu wengine wenye ujasiri waliendelea kutafsiri Biblia katika lugha nyingine, na hatua kwa hatua nuru ya kiroho ikaenea katika ulimwengu wote wenye giza.

  • Ibada Safi​—Yarudishwa Hatua kwa Hatua
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
      • William Tyndale akitafsiri Biblia.

        “Sauti ya vitu vinavyogongana”

        William Tyndale na watu wengine walitokeza tafsiri za Biblia katika Kiingereza na lugha nyingine

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki