-
“Mtakuwa Hai”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
9. Kuna ulinganifu gani kati ya mambo yaliyowapata Waisraeli wa kale wa asili na yaliyowapata “Israeli wa Mungu”?
9 Unabii kuhusu kurudishwa kwa Israeli, kama ule uliotolewa na Ezekieli, ulitimizwa kwa njia kubwa zaidi. (Mdo. 3:21) Kama vile taifa la kale la Israeli wa kimwili ‘lilivyouawa’ na kufa kwa njia ya kiroho kwa muda mrefu, ndivyo “Israeli wa Mungu,” kutaniko la Wakristo waliotiwa mafuta, lilivyouawa kwa njia ya mfano na kupatwa na utekwa ulio kama kifo kwa kipindi kirefu. (Gal. 6:16) Kwa kweli, utekwa wa kutaniko la watiwa mafuta kwa ujumla uliendelea kwa muda mrefu sana hivi kwamba hali yao ya kiroho ingeweza kulinganishwa na mifupa “mikavu sana.” (Eze. 37:2) Kama ilivyozungumziwa katika sura iliyotangulia, utekwa wa kutaniko la Wakristo waliotiwa mafuta ulianza karne ya pili W.K. na kuendelea kwa karne nyingi, kama vile Yesu alivyosema katika mfano wake wa ngano na magugu unaohusu Ufalme.—Mt. 13:24-30.
Mifupa “mikavu sana” ambayo Ezekieli aliona katika maono iliwakilisha kipindi kirefu cha utekwa unaofanana na kifo cha watiwa mafuta wa Mungu (Tazama fungu la 8 na 9)
-
-
“Mtakuwa Hai”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
a Mifupa ambayo Ezekieli aliona katika maono, haikuwa ya watu waliokufa kifo cha kawaida, bali ya “watu waliouawa.” (Eze. 37:9) “Watu wote wa nyumba ya Israeli” waliuawa kwa njia ya mfano wakati wakaaji wa ufalme wa Israeli wenye makabila kumi na wale wa ufalme wa Yuda wenye makabila mawili waliposhindwa, wakatekwa, na kupelekwa uhamishoni na Waashuru na Wababiloni.
-