Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 10, 11. (a) Leo, tunapata baraka gani zinazotiririka kama mto? (b) Baraka zinazotiririka kutoka kwa Yehova zimeongezekaje ili kutimiza uhitaji unaoongezeka katika siku za mwisho?

      10 Mto wa baraka. Maji yanayotiririka kutoka kwenye nyumba ya Yehova yanatukumbusha baraka gani leo? Kwa kweli, yanatukumbusha mambo mengi ambayo Yehova anatuandalia ili kutunufaisha kiroho. Jambo muhimu zaidi ni dhabihu ya fidia ya Kristo inayosafisha, ambayo hutuwezesha kupata msamaha wa dhambi. Kweli safi za Neno la Mungu zinalinganishwa pia na maji yanayoleta uhai, ambayo husafisha. (Efe. 5:25-27) Baraka hizo zimetiririkaje leo?

  • “Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 17 Mto wa baraka. Katika Paradiso, mto huo wa mfano utapanuka hata zaidi kwa kuwa utaleta baraka za kiroho na pia za kimwili. Wakati wa Utawala wa Miaka Elfu Moja wa Yesu, Ufalme wa Mungu utawasaidia watu waaminifu wafaidike na fidia kwa njia kubwa zaidi. Hatua kwa hatua, watakuwa wakamilifu! Hakutakuwa tena na magonjwa, madaktari, wauguzi, hospitali, wala bima ya afya! Maji hayo ya uzima yatatiririka kwa mamilioni watakaooka Har–Magedoni, yaani, “umati mkubwa” watakaotoka kwenye “dhiki kuu.” (Ufu. 7:9, 14) Hata hivyo, ingawa mwanzo huo wa kutiririka kwa mto wa baraka utakuwa wenye kustaajabisha, ni mdogo kwa kulinganishwa na mambo yatakayotokea baadaye. Kama inavyoonyeshwa na maono ya Ezekieli, mto huo utapanuka ili kutimiza uhitaji mkubwa zaidi.

      Watu wenye nguvu za ujana, wenye afya nzuri na furaha wakifanya kazi kwenye Paradiso. Mto unatiririka nyuma yao.

      Katika Paradiso, mto wa baraka utafanya kila mtu awe kijana na mwenye afya (Tazama fungu la 17)

  • Kijito Kinakuwa Mto Mkubwa!
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • Kijito Kinakuwa Mto Mkubwa!

      Ezekieli anaona kijito kinachotiririka kutoka katika hekalu la Yehova na baada ya kilomita mbili hivi kijito hicho kinakuwa mto wenye kina kirefu! Kwenye kingo za mto anaona miti yenye lishe na inayoponya iliyo na majani mengi. Mambo hayo yanamaanisha nini?

      Kijito kinatiririka kutoka hekalu la Yehova na kuwa mto mkubwa. Ishara zinaonyesha kina cha maji. Mikono 1,000: kufikia vifundo vya miguu. Mikono 2,000: kufikia magoti. Mikono 3,000: kufikia kiunoni. Mikono 4,000: kina kirefu kisichoweza kuvukwa kwa miguu.

      Mto Unaoleta Baraka

      ZAMANI: Baada ya wahamishwa kurudi kwenye nchi yao, walibarikiwa sana waliposhiriki katika kurudisha ibada safi hekaluni

      NYAKATI ZETU: Mwaka wa 1919 ibada safi ilirudishwa, na hivyo kufungua njia ili watumishi waaminifu wa Yehova wapate baraka nyingi sana za kiroho

      WAKATI UJAO: Baada ya Har–Magedoni, Yehova atatubariki sana kimwili na kiroho

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki