Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 2 Ezekieli anatambua kwamba mto huo unaingia kwenye Bahari ya Chumvi na kila mahali ambapo maji ya mto yanafika yanaponya maji yenye chumvi yasiyo na uhai, na kufanya yawe na samaki wengi. Kwenye kingo za mto, anaona miti mingi ya kila aina ikikua. Kila mwezi, inazaa matunda yenye lishe na kuchipua majani yanayoponya. Ezekieli anapoona mambo hayo yote, moyo wake unakuwa na amani na tumaini. Lakini sehemu hii ya maono ya hekalu ilimaanisha nini kwa Ezekieli na kwa wahamishwa wenzake? Na inamaanisha nini kwetu leo?

  • “Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 6. (a) Maono hayo ya kinabii yalitoa ahadi gani yenye kufariji? (b) Maono hayo pia yalitoa onyo gani? (Tazama maelezo ya chini.)

      6 Maji yanayoleta uhai. Katika maono ya Ezekieli, mto uliingia kwenye Bahari ya Chumvi, na kuponya sehemu kubwa ya bahari hiyo. Ona kwamba maji hayo yalitokeza samaki wengi wa aina mbalimbali kama samaki walio katika Bahari Kuu, yaani, Bahari ya Mediterania. Pia, kulikuwa na biashara kubwa ya uvuvi kwenye ufuo wa Bahari ya Chumvi katika miji miwili ambayo haikuwa imekaribiana sana. Malaika alisema: “Mahali ambapo kijito hicho kinapita, kila kitu kitaishi.” Je, hilo linamaanisha kwamba maji yanayotoka katika nyumba ya Yehova yalifika kila mahali katika Bahari ya Chumvi? Hapana. Malaika alieleza kwamba kulikuwa na sehemu zenye matope ambazo hazikufikiwa na maji yanayoleta uhai. Sehemu hizo ‘zingebaki zikiwa sehemu za chumvi.’b (Eze. 47:8-11) Basi maono hayo ya kinabii yalitoa ahadi yenye kufariji kwamba ibada safi ingewafanya watu wawe hai, na wasitawi. Lakini pia onyo hili lililotolewa: Si watu wote ambao wangekubali baraka za Yehova; wala si wote wangeponywa.

  • “Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 6. (a) Maono hayo ya kinabii yalitoa ahadi gani yenye kufariji? (b) Maono hayo pia yalitoa onyo gani? (Tazama maelezo ya chini.)

      6 Maji yanayoleta uhai. Katika maono ya Ezekieli, mto uliingia kwenye Bahari ya Chumvi, na kuponya sehemu kubwa ya bahari hiyo. Ona kwamba maji hayo yalitokeza samaki wengi wa aina mbalimbali kama samaki walio katika Bahari Kuu, yaani, Bahari ya Mediterania. Pia, kulikuwa na biashara kubwa ya uvuvi kwenye ufuo wa Bahari ya Chumvi katika miji miwili ambayo haikuwa imekaribiana sana. Malaika alisema: “Mahali ambapo kijito hicho kinapita, kila kitu kitaishi.” Je, hilo linamaanisha kwamba maji yanayotoka katika nyumba ya Yehova yalifika kila mahali katika Bahari ya Chumvi? Hapana. Malaika alieleza kwamba kulikuwa na sehemu zenye matope ambazo hazikufikiwa na maji yanayoleta uhai. Sehemu hizo ‘zingebaki zikiwa sehemu za chumvi.’b (Eze. 47:8-11) Basi maono hayo ya kinabii yalitoa ahadi yenye kufariji kwamba ibada safi ingewafanya watu wawe hai, na wasitawi. Lakini pia onyo hili lililotolewa: Si watu wote ambao wangekubali baraka za Yehova; wala si wote wangeponywa.

  • “Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • a Isitoshe, Wayahudi wahamishwa ambao walikumbuka mandhari ya kijiografia ya nchi yao inaelekea walijua kwamba mto huo haukuwa halisi kwa sababu ulitiririka kutoka hekaluni kwenye mlima mrefu sana, ambao kihalisi haukuwepo katika eneo lililotajwa. Pia, maono hayo yalidokeza kwamba mto huo ulitiririka moja kwa moja hadi kwenye Bahari ya Chumvi, jambo ambalo halingewezekana kulingana na mandhari ya kijiografia ya eneo hilo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki