-
“Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
2 Ezekieli anatambua kwamba mto huo unaingia kwenye Bahari ya Chumvi na kila mahali ambapo maji ya mto yanafika yanaponya maji yenye chumvi yasiyo na uhai, na kufanya yawe na samaki wengi. Kwenye kingo za mto, anaona miti mingi ya kila aina ikikua. Kila mwezi, inazaa matunda yenye lishe na kuchipua majani yanayoponya. Ezekieli anapoona mambo hayo yote, moyo wake unakuwa na amani na tumaini. Lakini sehemu hii ya maono ya hekalu ilimaanisha nini kwa Ezekieli na kwa wahamishwa wenzake? Na inamaanisha nini kwetu leo?
-
-
“Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
6. (a) Maono hayo ya kinabii yalitoa ahadi gani yenye kufariji? (b) Maono hayo pia yalitoa onyo gani? (Tazama maelezo ya chini.)
6 Maji yanayoleta uhai. Katika maono ya Ezekieli, mto uliingia kwenye Bahari ya Chumvi, na kuponya sehemu kubwa ya bahari hiyo. Ona kwamba maji hayo yalitokeza samaki wengi wa aina mbalimbali kama samaki walio katika Bahari Kuu, yaani, Bahari ya Mediterania. Pia, kulikuwa na biashara kubwa ya uvuvi kwenye ufuo wa Bahari ya Chumvi katika miji miwili ambayo haikuwa imekaribiana sana. Malaika alisema: “Mahali ambapo kijito hicho kinapita, kila kitu kitaishi.” Je, hilo linamaanisha kwamba maji yanayotoka katika nyumba ya Yehova yalifika kila mahali katika Bahari ya Chumvi? Hapana. Malaika alieleza kwamba kulikuwa na sehemu zenye matope ambazo hazikufikiwa na maji yanayoleta uhai. Sehemu hizo ‘zingebaki zikiwa sehemu za chumvi.’b (Eze. 47:8-11) Basi maono hayo ya kinabii yalitoa ahadi yenye kufariji kwamba ibada safi ingewafanya watu wawe hai, na wasitawi. Lakini pia onyo hili lililotolewa: Si watu wote ambao wangekubali baraka za Yehova; wala si wote wangeponywa.
-
-
Kijito Kinakuwa Mto Mkubwa!Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
Maji Yanayoleta Uhai
ZAMANI: Yehova aliwabariki sana watu wake watiifu, na walisitawi kiroho hata idadi yao ilipozidi kuongezeka
NYAKATI ZETU: Katika paradiso ya sasa ya kiroho inayoendelea kukua, watu wanaozidi kuongezeka wamefaidika na baraka za kiroho kutoka kwa Yehova zinazozidi kuongezeka na wamekuwa hai kwa njia ya kiroho
WAKATI UJAO: Wale watakaookoka Har–Magedoni wataungana na mamilioni ya watu watakaofufuliwa, na watu wote watapata baraka nyingi za Yehova
-
-
“Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
12. (a) Tumeona jinsi gani ujumbe wa kweli ukiwaletea watu uhai na afya ya kiroho? (b) Maono hayo yanatupatia onyo gani leo? (Pia, tazama maelezo ya chini.)
12 Maji yanayoleta uhai. Ezekieli aliambiwa: “Mahali ambapo kijito hicho kinapita, kila kitu kitaishi.” Fikiria jinsi ambavyo ujumbe wa kweli umetiririka kwa wote ambao wamekuja katika nchi yetu ya kiroho iliyorudishwa. Kweli za Biblia zimegusa mioyo ya mamilioni ya watu na kuwafanya wawe hai na wenye afya kiroho. Lakini maono hayo pia yanatoa onyo muhimu kwamba si watu wote wanaoendelea kufuata kweli hizo. Kama sehemu zenye majimaji na matope katika Bahari ya Chumvi kwenye maono ya Ezekieli, mioyo fulani inakuwa migumu, haikubali kweli na inakataa kuifuata.c Tusiwe hivyo kamwe!—Soma Kumbukumbu la Torati 10:16-18.
-