Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 7. Miti iliyo kwenye kingo za mto katika maono iliwapa Wayahudi waliohamishwa uhakikisho gani?

      7 Miti kwa ajili ya chakula na kuponya. Namna gani miti iliyokuwa kwenye kingo za mto? Inafanya maono hayo yapendeze zaidi, sivyo? Pia, inaongeza maana ya maono hayo. Kwa hakika, Ezekieli na Wayahudi wenzake walifurahia kufikiria kuhusu matunda matamu ya miti hiyo, ambayo ingezaa kila mwezi! Unabii huo wenye kuvutia uliwahakikishia kwamba Yehova angewalisha kiroho. Uliwahakikishia jambo gani lingine? Ona kwamba majani ya miti hiyo ‘yangetumiwa kuponya.’ (Eze. 47:12) Yehova alijua kwamba kuliko jambo lingine lolote, wahamishwa waliorudishwa wangehitaji kuponywa kiroho, na aliahidi kufanya hivyo. Unabii mwingine wa kurudishwa ulionyesha jinsi alivyofanya hivyo, kama tulivyoona kwenye Sura ya 9 ya kitabu hiki.

  • Kijito Kinakuwa Mto Mkubwa!
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • Miti kwa Ajili ya Chakula na Kuponya

      ZAMANI: Kwa njia ya kiroho, Yehova aliwalisha watu wake waaminifu katika nchi yao iliyorudishwa; pia aliwaponya ugonjwa wa kiroho waliokuwa nao kwa muda mrefu

      NYAKATI ZETU: Chakula kingi cha kiroho kinawasaidia watu wakabiliane na ugonjwa na njaa ya kiroho iliyoenea ulimwenguni leo

      WAKATI UJAO: Kristo na watawala wenzake 144,000 watawasaidia wanadamu watiifu wafikie ukamilifu na kufurahia afya bora na nguvu milele!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki