-
‘Mtaigawa Nchi Iwe Urithi’Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
‘Mmegawiwa Nchi Hii Iwe Urithi Wenu’
5, 6. (a) Katika maono ya Ezekieli ni nchi gani waliyopaswa kuigawa? (Tazama picha mwanzoni mwa sura hii.) (b) Maono kuhusu kugawa nchi yalikuwa na kusudi gani?
5 Soma Ezekieli 47:14. Katika maono, Yehova alimwonyesha Ezekieli sehemu ya nchi ambayo baadaye ingekuwa kama “bustani ya Edeni.” (Eze. 36:35) Kisha Yehova akasema: “Hili ndilo eneo ambalo mtayagawia yale makabila 12 ya Israeli kuwa urithi wao wa ardhi.” (Eze. 47:13) “Eneo” ambalo wangegawiwa lilikuwa nchi ya Israeli iliyorudishwa ambako wahamishwa wangerudishwa. Baadaye, kama ilivyoandikwa kwenye Ezekieli 47:15-21, Yehova alifafanua kwa undani mipaka hususa ya nchi yote.
6 Maono hayo ya kuigawa nchi yalikuwa na kusudi gani? Ufafanuzi wa vipimo hususa vya mipaka ulimhakikishia Ezekieli na wahamishwa wenzake kwamba kwa hakika nchi yao waliyoipenda ingerudishwa. Wazia jinsi ambavyo uhakikisho huo kutoka kwa Yehova, wenye habari nyingi na maelezo yaliyo wazi, ulivyowatia moyo wahamishwa hao! Je, kweli watu hao wa Mungu waligawiwa urithi katika nchi waliyopewa? Ndiyo.
7. (a) Ni matukio gani yaliyoanza mwaka wa 537 K.W.K., na yanatukumbusha nini? (b) Tutachunguza swali gani kwanza?
7 Mwaka wa 537 K.W.K., miaka 56 hivi baada ya Ezekieli kupata maono, maelfu ya wahamishwa walianza kurudi katika nchi ya Israeli na kuimiliki. Matukio hayo makubwa ya zamani yanatukumbusha jambo kama hilo ambalo wakati wetu limekuwa likitokea kati ya watu wa Mungu. Kwa njia fulani, wao pia walipokea urithi wa nchi. Jinsi gani? Yehova aliwaruhusu watu wake waingie katika nchi ya kiroho na kuimiliki. Kwa hiyo, kurudishwa kwa Nchi ya Ahadi zamani kunatufundisha mengi kuhusu kurudishwa kwa nchi ya kiroho ya watu wa Mungu leo. Lakini kabla ya kuchunguza mambo hayo, acheni kwanza tujibu swali hili, “Kwa nini tunaweza kusema kwamba kwa kweli leo kuna nchi ya kiroho?”
8. (a) Yehova alichagua taifa gani baada ya kuwakataa Waisraeli wa asili? (b) Nchi, au paradiso ya kiroho ni nini? (c) Ilianzishwa lini, na ni nani wanaoishi humo?
8 Katika maono ambayo Ezekieli aliona awali, Yehova alionyesha kwamba unabii kuhusu kurudishwa kwa Israeli ungetimizwa kwa njia kubwa zaidi baada ya ‘mtumishi wake Daudi,’ yaani, Yesu Kristo, kuanza kutawala akiwa Mfalme. (Eze. 37:24) Jambo hilo lilitokea mwaka wa 1914 W.K. Kufikia wakati huo, muda mrefu ulikuwa umepita tangu Waisraeli wa asili walipoacha kuwa watu wa Mungu na nafasi yao kuchukuliwa na taifa la Israeli wa kiroho, lililofanyizwa na Wakristo waliotiwa mafuta. (Soma Mathayo 21:43; 1 Petro 2:9.) Hata hivyo, Yehova hakulikataa tu taifa la asili la Israeli na kuanzisha taifa la kiroho bali pia aliikataa nchi halisi ya Israeli na kuanzisha nchi, au paradiso ya kiroho. (Isa. 66:8) Kama tulivyoona katika Sura ya 17 ya kitabu hiki, nchi ya kiroho ni mazingira salama ya kiroho, au mahali pa utendaji, ambapo watiwa mafuta waliobaki wamekuwa wakimwabudu Yehova tangu mwaka wa 1919. (Tazama sanduku la 9B, “Kwa Nini 1919?”) Muda ulipozidi kupita, wale walio na tumaini la kuishi duniani, yaani, “kondoo wengine,” walianza pia kuingia katika nchi hiyo ya kiroho. (Yoh. 10:16) Ingawa paradiso ya kiroho inazidi kukua na kupanuka leo, baraka zake zitaonekana kikamili baada ya Har–Magedoni.
-
-
‘Mtaigawa Nchi Iwe Urithi’Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
13 Kwanza, nchi. Musa aliagizwa ayagawie makabila makubwa eneo kubwa kuliko makabila madogo. (Hes. 26:52-54) Hata hivyo, katika maono ya Ezekieli, Yehova alitoa maagizo hususa ya kuyagawia urithi makabila yote “kwa usawa [“kila mtu kama ndugu yake,” maelezo ya chini].” (Eze. 47:14) Basi umbali kutoka mpaka wa kaskazini hadi mpaka wa kusini katika urithi wa kila kabila ulipaswa kulingana katika maeneo yote 12. Waisraeli wote—bila kuzingatia kabila lao—wangepata kwa usawa mazao mengi ambayo yangetokezwa na Nchi ya Ahadi yenye maji mengi.
-