Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yesu Kristo
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
    • Uthibitisho wa huduma ya miaka mitatu na nusu. Kauli iliyo dhahiri zaidi inaweza kukatwa kupitia uthibitisho uliosalia wa kronolojia. Uthibitisho huu unahusiana na urefu wa huduma ya Yesu na wakati wa kifo chake. Unabii kwenye Danieli 9:24-27 (unazungumziwa kikamili katika makala SEVENTY WEEKS) unaelekeza kuwa kutokea kwa Masihi ni mwanzoni mwa “juma” la 70 la miaka (Da 9:25) na kifo chake cha dhabihu katikati ya “nusu” ya juma la mwisho, na hivyo kukomesha uhalali wa dhabihu na matoleo ya zawadi chini ya agano la Sheria. (Da 9:26, 27; linganisha Ebr 9:9-14; 10:1-10.) Hii ingemaanisha huduma ya kipindi cha miaka mitatu na nusu (nusu ya “juma” la miaka saba) kwa ajili ya Yesu Kristo.

  • Yesu Kristo
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
    • Muhtasari wa uthibitisho. Basi, kwa muhtasari, kwa kuwa kifo cha Yesu kilitukia katika mwezi wa masika wa Nisani, lazima huduma yake, ambayo ilianza miaka mitatu na nusu kabla ya hapo kulingana na Danieli 9:24-27, iwe ilianza katika vuli, karibu na mwezi wa Ethanimu (Septemba-Oktoba). Kwa hiyo, lazima huduma ya Yohana (iliyoanza katika mwaka wa 15 wa Tiberio), iwe ilianza katika masika ya mwaka 29 W.K. Kwa hiyo kuzaliwa kwa Yohana kungekuwa katika masika ya mwaka 2 K.W.K., kuzaliwa kwa Yesu kungekuja kama miezi sita baadaye katika vuli ya 2 K.W.K., huduma yake ingeanza miaka 30 baadaye katika vuli ya 29 W.K., na kifo chake kingekuja katika mwaka 33 W.K. (siku ya Nisani 14 katika masika, kama ilivyotajwa).

  • Majuma Sabini
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
    • Agano kutendeshwa “kwa juma moja.” Danieli 9:27 lasema hivi: “Naye ataendelea kulitendesha agano kwa ajili ya wengi kwa juma moja [au miaka saba]; na katika nusu ya juma hilo atakomesha dhabihu na toleo la zawadi.” Haingewezekana “agano” liwe lilikuwa ni lile agano la Sheria, kwa maana miaka mitatu na nusu baada ya kuanza lile “juma” la 70, dhabihu ya Kristo ilisababisha hilo liondolewe na Mungu: “Yeye ameiondoa [ile Sheria] njiani kwa kuipigilia misumari juu ya mti wa mateso.” (Kol 2:14) Pia, “Kristo kwa kutununua alituachilia huru kutoka katika laana ya Sheria . . . Kusudi lilikuwa kwamba baraka ya Abrahamu ije kupitia Yesu Kristo kwa ajili ya mataifa.” (Gal 3:13, 14) Mungu, kupitia Kristo, alipanua baraka za agano la Abrahamu zifikie uzao wa asili wa Abrahamu, bila kutia ndani Watu wa Mataifa hadi Injili ilipopelekwa kwao kupitia mahubiri ya Petro kwa Kornelio Mwitalia. (Mdo 3:25, 26; 10:1-48) Kugeuzwa imani huku kwa Kornelio na nyumba yake kulitokea baada ya kugeuzwa imani kwa Sauli wa Tarso, ambako kijumla hufikiriwa kulitokea karibu na mwaka 34 W.K.; baada ya hilo kutaniko lilifurahia kipindi cha amani, likiwa linajengwa. (Mdo 9:1-16, 31) Basi, inaonekana kwamba kuingizwa kwa Kornelio ndani ya kutaniko la Kikristo kulitokea karibu na vuli ya mwaka 36 W.K., ambao ungekuwa ndio mwisho wa lile “juma” la 70, ikiwa ni miaka 490 tangu 455 K.W.K

      Dhabihu na matoleo ‘yakomeshwa.’ Usemi ‘kukomeshwa,’ unaotumiwa kurejelea dhabihu na toleo la zawadi, wamaanisha, kihalisi, “kusababisha au kufanya sabato, kupumzika, kuacha kufanya kazi.” Zile “dhabihu na toleo la zawadi” ambazo ‘zinakomeshwa,’ kulingana na Danieli 9:27, hazingeweza kuwa ni fidia ya dhabihu ya Yesu, wala kwa kufikiri vizuri hazingeweza kuwa ni dhabihu yoyote ya kiroho yenye kutolewa na wafuasi wa nyayo zake. Lazima ziwe zinarejelea dhabihu na matoleo ya zawadi yaliyotolewa na Wayahudi kwenye hekalu katika Yerusalemu kulingana na Sheria ya Musa.

      “Nusu ya juma hilo” ingekuwa katikati ya miaka saba, au baada ya miaka mitatu na nusu ndani ya hilo “juma” la miaka. Kwa kuwa “juma” la 70 lilianzia karibu vuli ya mwaka 29 W.K. wakati wa ubatizo wa Yesu na kutiwa mafuta awe Kristo, nusu ya juma hilo (miaka mitatu na nusu) ingeendelea hadi masika ya 33 W.K., au wakati wa Pasaka (Nisani 14) ya mwaka huo. Inaonekana siku hiyo ilikuwa ni Aprili 1, 33 W.K., kulingana na kalenda ya Gregory. (Ona LORD’S EVENING MEAL [Time of Its Institution].) Mtume Paulo anatuambia kwamba Yesu alikuja ‘kufanya mapenzi ya Mungu,’ mapenzi ambayo yalikuwa ni ‘kuondolea mbali lile la kwanza [dhabihu na matoleo kulingana na ile Sheria] ili asimamishe lile la pili.’ Alifanya jambo hilo kwa kutoa mwili wake mwenyewe kuwa dhabihu.—Ebr 10:1-10.

      Ijapokuwa makuhani wa Kiyahudi waliendelea kutoa dhabihu kwenye hekalu katika Yerusalemu hadi lilipoangamizwa katika 70 W.K., kwa Mungu dhabihu hizo kwa ajili ya dhambi ziliacha kuwa zenye kukubalika na kuwa halali. Kabla tu ya kifo chake, Yesu aliliambia Yerusalemu hivi: “Nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa.” (Mt 23:38) Kristo “alitoa dhabihu moja kwa ajili ya dhambi daima . . . Kwa maana ni kwa toleo moja la dhabihu kwamba yeye amewafanya wale wanaotakaswa wawe wakamilifu daima.” “Sasa mahali palipo na msamaha [wa dhambi na vitendo vya ukosefu wa sheria] wa mambo hayo, hapana tena toleo kwa ajili ya dhambi.” (Ebr 10:12-14, 18) Mtume Paulo anataja kwamba unabii wa Yeremia ulisema juu ya agano jipya, kwa hivyo, lile agano lililotangulia (agano la Sheria) likiwa halitendi tena na kuchakaa, lilikuwa “karibu kutoweka.”—Ebr 8:7-13.

  • Majuma Sabini
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
    • Maangamizi kwenye jiji hilo na mahali patakatifu. Iilikuwa baada ya “majuma” 70, lakini likiwa tokeo la moja kwa moja la Wayahudi kumkataa Kristo wakati wa lile “juma” la 70, matukio ya sehemu za mwisho za Danieli 9:26 na 27 yalitimizwa. Maandishi ya historia yanaonyesha kwamba Tito mwana wa Maliki Vepasiani wa Roma alikuwa ndiye kiongozi wa vikosi vya Roma vilivyokuja dhidi ya Yerusalemu. Kwa kweli majeshi hayo yaliingia ndani ya Yerusalemu na hekalu lenyewe, kama mafuriko, na kuliangamiza jiji hilo na hekalu lake. Kusimama huku kwa majeshi ya kipagani katika mahali patakatifu kuliyafanya yawe “chukizo.” (Mt 24:15) Jitihada zote zilizofanywa kabla ya mwisho wa Yerusalemu ili kunyamazisha hali hiyo zilishindwa kwa sababu amri ya Mungu ilikuwa ni hii: “Kilichoamuliwa ni ukiwa,” na “mpaka maangamizi, kitu kile kilichoamuliwa kitamwagika pia juu ya yule anayekaa ukiwa.”

      Maoni ya Kiyahudi. Maandishi-matini ya Masora, yenye mfumo wake wa nukta za irabu, yalitayarishwa katika sehemu ya mwisho ya nusu ya milenia ya kwanza W.K. Ni wazi kwa sababu ya kumkataa Yesu Kristo kuwa Masihi, Wamasora walitia alama ya mkazo kwenye maandishi-matini ya Kiebrania kwenye Daniel 9:25 wakiweka ʼath·nach′, au “kituo cha kikomo,” baada ya “majuma saba,” kwa jambo hilo wakagawanya hilo na yale “majuma 62”; katika njia hiyo yale majuma 62 ya unabii, yaani, miaka 434, yanaonekana kuhusu wakati wa kujenga upya Yerusalemu la kale. Tafsiri ya Isaac Leeser inasema hivi: “Basi ujue na kuelewa, kwamba tangu kutoka kwa neno la kurudisha na kujenga Yerusalemu hadi mtiwa-mafuta aliye mkuu kutakuwa majuma saba: [kituo cha kikomo hapa kinawakilishwa na nukta mbili] na wakati wa majuma sitini na mawili ndipo litakapojengwa tena likiwa na barabara na mahandaki (kulizunguka), naam katika mikazo ya nyakati hizo.” Tafsiri ya Chama cha Uchapishaji cha Kiyahudi cha Marekani yasema vivyo hivyo: “kutakuwa majuma saba; na kwa majuma makumi sita na mawili, litajengwa tena.” Katika tafsiri hizi mbili (katika Kiingereza) maneno “wakati” na “kwa,” yanaonekana katika tafsiri ya Kiingereza, bila shaka ili yaunge mkono fasiri ya watafsiri hao.

      Profesa E. B. Pusey, katika kielezi-chini kimoja katika mojawapo mihadhara yake iliyotolewa kwenye Chuo Kikuu cha Oxford, anatoa maelezo haya juu ya utiaji alama za mkazo za Wamasora: “Wayahudi walitia kituo kikuu cha mstari huo chini ya שׁבעה [saba], wakikusudia kutenganisha hizo namba mbili, 7 na 62. Lazima wawe walifanya hivyo kwa udanganyifu, למען המינים (kama Rashi [Rabi maarufu wa Kiyahudi wa karne ya 11 na ya 12 W.K.] anavyosema katika kukataa mafafanuzi halisi yaliyowafaa Wakristo) ‘kwa sababu ya wazushi,’ yaani, Wakristo. Kwa kishazi hicho cha mwisho, kugawanywa hivyo, ingeweza kumaanisha tu, ‘na wakati wa majuma makumi sita na mawili barabara na ukuta vitarudishwa na kujengwa,’ yaani, kwamba Yerusalemu lingechukua miaka 434 kujengwa upya, jambo ambalo lingekuwa ni upuuzi.”—Daniel the Prophet, 1885, ukur. 190.

      Kwa habari ya Danieli 9:26 (Le), ambalo lasema hivi, kwa sehemu, “Na baada ya yale majuma-sitini na mwili ndipo mtiwa-mafuta atakapokatiliwa mbali bila kuwa na mwandamizi mwenye kumfuata,” Wafafanuzi wa Kiyahudi hutumia hayo majuma 62 kufikia kipindi cha enzi za Wamakabayo, na usemi “mtiwa-mafuta” kumhusu Mfalme Agripa wa 2, aliyeishi wakati wa kuangamizwa kwa Yerusalemu, 70 W.K. Au wengine husema huyo alikuwa kuhani mkuu, Oniasi, aliyepinduliwa na Antioko Epifane katika 175 K.W.K Matumizi yao ya unabii huo kuhusu mojawapo kati ya wanaume hao yangekuwa yenye kuukosesha umuhimu au maana yoyote iliyo halisi, na tofauti hiyo katika kukadiria tarehe ingefanya yale majuma 62 yawe unabii usio na wakati ulio sahihi hata kidogo.—Ona Soncino Books of the Bible (ufafanuzi juu ya Da 9:25, 26), kilichofanyiwa uhariri na A. Cohen, London, 1951.

      Katika jitihada ya kutetea maoni yao, wasomi hao wa Kiyahudi husema kwamba yale “majuma saba” si 7 mara 7, au miaka 49, bali ni miaka 70; na huku wanahesabu yale majuma 62 kuwa 7 mara miaka 62. Wanadai hilo lilirejelea kile kipindi cha uhamisho wa Babiloni. Wanamfanya Koreshi au Zerubabeli au Kuhani Mkuu Yeshua awe “mtiwa-mafuta” katika mstari huu (Da 9:25), na huku yule “mtiwa-mafuta” katika Danieli 9:26 akiwa mtu mwingine.

      Inaweza kuangaliwa, kuhusiana na hilo, kwamba tafsiri ya Septuajinti, iliyofanywa na wasomi wa Kiyahudi katika karne tatu za kwanza K.W.K, yasema hivi, kwenye Danieli 9:25, “Tangu kutolewa kwa amri ya kujibu na kujengwa kwa Yerusalemu hadi Kristo aliye mkuu kutakuwa majuma saba, na majuma sitini na mawili: kisha ule wakati utarudi, na barabara itajengwa, na ukuta.” (LXX, Bagster) Kwa sehemu, Septuagint ya Thompson inasema hivi: “majuma saba, na majuma sitini na mawili. Hakika wao watarudi na barabara itajengwa na ukuta.”

      Tafsiri zilizo nyingi za Kiingereza hapa hazifuati alama za maandishi za Wamasora. Ama zina alama ya mkato baada ya usemi “majuma saba” au katika matumizi ya maneno zinaonyesha kwamba yale majuma 62 yanafuata yale 7 yakiwa sehemu ya yale 70, nazo hazionyeshi kwamba yale majuma 62 yanahusu kile kipindi cha kujenga upya Yerusalemu. (Linganisha Da 9:25 katika UV, AT, Dy, NW, Ro, Yg.) Taarifa ya mhariri ya James Strong katika Commentary on the Holy Scriptures cha Lange (Da 9:25, klz-chn, ukur. 198) yasema hivi: “Hoja pekee ya tafsiri hii, ambayo inatenganisha vile vipindi viwili vya majuma saba na majuma sitini na mawili, ikionyesha hayo ya kwanza kuwa ndio wakati wa kuwasili kwa Mkuu aliye Mtiwa-Mafuta, na hayo ya mwisho kuwa ndio upeo wa wakati wa kujenga upya, ni alama za maandishi za Wamasora, ambazo zinatia ile alama ya nukta katikati yake. . . . na tafsiri inayohusika inatia ndani muundo usiofaa wa sehemu ya pili, bila kihusishi. Kwa hiyo, ni afadhali zaidi, na ni sahili zaidi, kushikilia chapa ya Authorized Version, inayofuata tafsiri nyinginezo zote za kale.”—Kimetafsiriwa na kufanyiwa uhariri (Kiingereza) na P. Schaff, 1976.

      Maoni mengine mengi, mengine yakiwa ni ya Kimasihi na mengine yasiyokuwa ya Kimasihi, yametolewa kuhusu ni nini maana ya unabii huo. Mengine hujaribu kubadili utaratibu wa vipindi hivyo vya wakati wa unabii huo, huku mengine yakiyafanya yaende sambamba au kukanusha kwamba yana wakati halisi wa utimizo. Pia, kumekuwa na jitihada nyingi za kufanya matukio hayo yaliyotajwa yafae kipindi cha Wamakabayo au hata wakati wa kumalizia wa mwisho. Lakini wale wanaotokeza maoni hayo wanajiingiza katika utata mkubwa, na jitihada zao za kujinasua huwaingiza katika upumbavu au ukanushaji wa moja kwa moja kwamba unabii huo umeongozwa kwa roho au ni wa kweli. Kuhusu maoni hayo ya mwisho hasa, ambayo hutokeza matatizo mengi zaidi kuliko yale ambayo husuluhishwa nayo, msomi huyo aliyetangulia kutajwa, E. B. Pusey, anaeleza hivi: “Hayo ndiyo yaliyokuwa matatizo yasiyowezekana kusuluhishwa na ukosaji imani; ilibidi huo ujifanyie suluhisho, jambo ambalo, kufikia hapa, ndilo lililokuwa rahisi zaidi; kwa maana hapana lisilowezekana kuaminiwa na ukosefu wa imani, isipokuwa yale anayofunua Mungu.”—Ukur. 206.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki