Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Alijifunza Kuwa Mwenye Rehema
    Igeni Imani Yao
    • 20 Mungu alizungumza na Yona na kumwambia nabii huyo kwamba alikuwa anasikitikia mmea tu ambao ulisitawi usiku mmoja, na ambao Yona hakuwa ameupanda wala kuukuza. Kisha Mungu akamalizia hivi: “Kwa upande wangu, je, sipaswi kusikitikia Ninawi lile jiji kubwa, ambalo lina wanadamu zaidi ya 120,000 wasiojua hata kidogo tofauti kati ya mkono wao wa kuume na wa kushoto, na tena wanyama wengi wa kufugwa?”​—Yona 4:10, 11.c

      21. (a) Yehova alimfundisha Yona somo gani? (b) Simulizi la Yona linawezaje kutusaidia kujichunguza kwa unyoofu?

      21 Je, unaelewa maana ya mfano ambao Yehova alitumia? Yona hakuwa amefanya chochote ili kuutunza mmea huo. Kwa upande mwingine, Yehova alikuwa amewapa Waninawi uhai na aliwategemeza kama anavyowategemeza viumbe wote duniani. Yona angewezaje kuthamini zaidi mmea mmoja kuliko maisha ya wanadamu 120,000, pamoja na wanyama wao wote wa kufugwa? Ni kwa sababu Yona alifikiri kwa njia ya kibinafsi. Alisikitikia mmea huo kwa sababu ulikuwa umemnufaisha yeye mwenyewe. Vivyo hivyo, aliwakasirikia Waninawi kwa sababu za kibinafsi. Alitamani kuheshimiwa, na kutoonekana kuwa mwongo. Simulizi la Yona linaweza kutusaidia tujichunguze kwa unyoofu. Sote tuna mwelekeo wa kutenda kwa ubinafsi. Tunathamini sana kwamba Yehova anatufundisha kwa subira kutokuwa na ubinafsi, na pia kuonyesha hata zaidi huruma na rehema!

  • Alijifunza Kuwa Mwenye Rehema
    Igeni Imani Yao
    • c Mungu aliposema kwamba watu hao hawakujua tofauti kati ya kuume na kushoto alimaanisha kwamba hawakujua sheria za Mungu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki