-
‘Fanyeni Hivi kwa Kunikumbuka Mimi’Mnara wa Mlinzi—2013 | Desemba 15
-
-
9. Baadhi ya watu wana maoni gani yasiyo sahihi kuhusu mkate aliotumia Yesu?
9 Baadhi ya wanadini wanaamini kwamba Yesu aliposema: ‘Huu ni mwili wangu,’ mkate ulibadilika kimuujiza na kuwa mwili wake halisi. Hata hivyo, jambo hilo si kweli.a Mwili huo, yaani, Yesu mwenyewe alikuwa mbele ya mitume wake waaminifu, na mkate usiotiwa chachu ambao wangekula ulikuwa pia mbele yao. Ni wazi kwamba Yesu alikuwa akiongea kwa kutumia mfano kama alivyofanya mara nyingi.—Yoh. 2:19-21; 4:13, 14; 10:7; 15:1.
10. Ni nini kinachofananishwa na mkate unaotumiwa katika Mlo wa Jioni wa Bwana?
10 Mkate huo ambao mitume wangeula ulimaanisha mwili wa Yesu. Mwili gani? Zamani, watumishi wa Mungu walifikiri kwamba kwa kuwa Yesu alivunja mkate lakini hakuna mfupa wake uliovunjwa, basi mkate ulimaanisha “mwili wa Kristo,” yaani, kutaniko la watiwa-mafuta. (Efe. 4:12; Rom. 12:4, 5; 1 Kor. 10:16, 17; 12:27) Hata hivyo, baada ya kufanya utafiti na kuchunguza Maandiko, walielewa kwamba mkate unafananisha mwili wa kibinadamu wa Yesu aliotayarishiwa. Yesu “aliteseka katika mwili,” na hata alitundikwa mtini. Kwa hiyo, katika Mlo wa Jioni wa Bwana, mkate unafananisha mwili wa kibinadamu wa Yesu ‘aliochukulia dhambi zetu.’—1 Pet. 2:21-24; 4:1; Yoh. 19:33-36; Ebr. 10:5-7.
-
-
‘Fanyeni Hivi kwa Kunikumbuka Mimi’Mnara wa Mlinzi—2013 | Desemba 15
-
-
15, 16. Mkate hutumiwa namna gani katika Mlo wa Jioni wa Bwana?
15 Mwishoni mwa hotuba, msemaji atataja kwamba wakati umefika wa kufanya kama Yesu alivyowaagiza mitume wake wafanye. Kama ilivyotajwa mwanzoni, mifano miwili itatumiwa, yaani, mkate usiotiwa chachu na divai nyekundu. Huenda mifano hiyo ikawekwa mezani karibu na msemaji. Msemaji atazungumzia simulizi la Biblia linaloonyesha mambo ambayo Yesu alisema na kufanya alipoanzisha mwadhimisho huo. Kwa mfano, tunasoma hivi katika simulizi la Mathayo: “Yesu alichukua mkate na, baada ya kutoa baraka, akaumega, akawapa wanafunzi, akasema: ‘Chukueni, mle. Huu unamaanisha mwili wangu.’” (Mt. 26:26) Yesu aliumega mkate huo usiotiwa chachu na kuwapa mitume waliokuwa kando yake. Katika ukumbusho utakaofanywa Aprili 14, utaona vipande vichache vya mikate isiyotiwa chachu vikiwa kwenye sahani.
-