Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zawadi Zilizofaa Mfalme
    Mnara wa Mlinzi—2015 | Machi 1
    • Vikolezo mbalimbali vyenye harufu nzuri

      Zawadi Zilizofaa Mfalme

      “Wanajimu kutoka sehemu za Mashariki . . . wakafungua hazina zao na kumtolea zawadi—dhahabu na ubani na manemane.”—Mathayo 2:1, 11.

      UNGEPENDA kumpa zawadi gani mtu aliye muhimu sana kwako? Katika nyakati za Biblia baadhi ya vikolezo vilikuwa na thamani kama dhahabu—thamani kubwa sana iliyomfaa mfalme.a Hii ndiyo sababu vikolezo vyenye harufu nzuri vilikuwa miongoni mwa zawadi ambazo wanajimu walileta kwa “mfalme wa wayahudi.”—Mathayo 2:1, 2, 11.

      Mafuta ya zeri

      Mafuta ya zeri

      Biblia inasema hivi pia kuhusu malkia wa Sheba alipofunga safari kumtembelea Mfalme Sulemani: “Ndipo akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, na mafuta ya zeri kwa wingi sana, na mawe ya thamani; na kulikuwa hakujapata kuwa na mafuta ya zeri kama yale ambayo malkia wa Sheba alimpa Mfalme Sulemani.”b (2 Mambo ya Nyakati 9:9) Pia wafalme walimpelekea Sulemani mafuta ya zeri ili kumtakia mema.—2 Mambo ya Nyakati 9:23, 24.

      Kwa nini vikolezo hivyo na vitu vilivyotengenezwa kwa vikolezo hivyo, vilikuwa vyenye thamani na gharama kubwa sana katika nyakati za Biblia? Kwa sababu vilitumiwa katika urembo, dini, na mazishi. (Tazama sanduku “Matumizi ya Vikolezo Vyenye Harufu Nzuri Katika Nyakati za Biblia.”) Mbali na kwamba vikolezo hivyo vilihitajiwa sana, viliuzwa bei ghali kwa sababu ya gharama za usafirishaji na upatikanaji.

      KUVUKA JANGWA LA ARABIA

      Kida

      Kida

      Katika nyakati za Biblia, baadhi ya mimea ya vikolezo ilisitawi kwenye Bonde la Yordani. Hata hivyo, vikolezo vingine vililetwa kutoka nchi nyingine. Biblia imetaja vikolezo vya aina mbalimbali. Vikolezo vinavyotajwa vinatia ndani waridi, udi, mafuta ya zeri, mdalasini, ubani, na manemane. Zaidi ya hayo, kulikuwa na vikolezo vingine vya chakula kama vile bizari, mnanaa, na dili.

      Vikolezo hivyo vilitoka wapi? Udi, kida, na mdalasini vilipatikana katika nchi za leo za China, India, na Sri Lanka. Vikolezo kama vile ubani na manemane vilitokana na miti na mimea ambayo ilisitawi katika maeneo ya jangwa kuanzia Arabia kusini hadi Somalia iliyo Afrika. Nardo, kilikuwa kikolezo cha pekee kilichotoka India katika maeneo ya Himalaya.

      Zafarani

      Zafarani

      Ili kufika Israeli, vikolezo vingi vilisafirishwa kupitia Arabia. Kwa sababu hiyo, katika milenia ya kwanza na ya pili K.W.K., Arabia ilikuja kuwa “msambazaji mkuu wa bidhaa hizo kati ya Mashariki na Magharibi,” kikasema kitabu The Book of Spices. Miji ya kale, ngome, na vituo vya safari vilivyo katika eneo la Negev kusini mwa Israel vinaonyesha njia walizotumia wafanyabiashara wa vikolezo hivyo. Shirika la World Heritage Centre la UNESCO liliripoti kwamba makazi hayo “yalichangia faida kubwa ya biashara hiyo  . . . kutoka Arabia kusini hadi Mediterania.”

      “Kiwango kidogo kiliuzwa kwa bei ghali, na kwa kuwa watu wengi walivipenda sana, vikolezo vilitumiwa kufanya biashara.” —The Book of Spices

      Kwa kawaida msafara uliobeba vikolezo hivyo vyenye harufu nzuri ulisafiri umbali wa kilometa 1,800 hivi ukipitia Arabia. (Ayubu 6:19) Biblia inataja msafara wa wafanyabiashara Waishmaeli waliokuwa wamebeba “ubani mweusi na zeri na gome lenye utomvu” kutoka Gileadi hadi Misri.” (Mwanzo 37:25) Wana wa Yakobo walimuuza ndugu yao Yosefu awe mtumwa kwa wafanyabiashara hao.

  • Zawadi Zilizofaa Mfalme
    Mnara wa Mlinzi—2015 | Machi 1
    • Aina Mbili ya Vikolezo Alivyopewa Yesu

      Ubani na manemane vilitokana na gundi ya utomvu ambayo hutengenezwa kwa utomvu wa gome la mti mdogo au mimea ya miiba.

      Mti wa ubani ulisitawi katika maeneo ya pwani ya kusini ya Arabia, na manemane ilisitawi vizuri katika inchi zenye maeneo makavu ambazo leo ni Somalia na Yemen. Vikolezo hivyo vilikuwa na thamani kubwa sana kwa sababu ya harufu yake. Yehova aliagiza vikolezo hivyo vitumiwe katika ibada yake—manemane ilitumiwa kutengeneza mafuta matakatifu, na ubani ulitumiwa kutengeneza uvumba mtakatifu. (Kutoka 30:23-25, 34-37) Hata hivyo,vikolezo hivyo vilitumiwa kwa njia nyingine.

      Kwa kawaida ubani uliotumiwa kama uvumba ulichomwa ili kutokeza harufu nzuri. Utomvu wa manemane ulitumiwa moja kwa moja. Manemane imetajwa mara tatu katika simulizi la Yesu: ikiwa zawadi aliyopewa alipokuwa mtoto (Mathayo 2: 11), alipokuwa katika mti wa mateso, alipewa divai iliyotiwa manemane ili apunguze maumivu (Marko 15:23), na ilikuwa mojawapo ya vikolezo vilivyotumiwa kuutayarisha mwili wake kwa ajili ya maziko (Yohana 19:39).

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki