-
Dhihirisha Itibari Katika Yehova kwa Kuzoea Mambo UliyojifunzaMnara wa Mlinzi—1988 | Agosti 15
-
-
11. Ni jinsi gani watu fulani wamenaswa katika ufuatiaji wa vitu vya kimwili, na kwa nini hili si jambo la hekima?
11 “Endeleeni, basi kutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake, na vitu vingine vyote hivi vitaongezwa kwenu ninyi.” (Mathayo 6:33, NW) Inasikitisha kama nini wakati watu fulani hawasikizi maneno hayo! Kwa kuimeza ile hekaya ya kujitafutia usalama wa kipesa, wao wanafuatia kwa ari utajiri, elimu ya kimwili, na kazi-maisha za kilimwengu, “wakiitibari katika njia yao ya kujidumisha.” (Zaburi 49:6, NW) Sulemani anaonya hivi: “Usijitaabishe ili kupata utajiri . . . Je! utavikazia macho vile ambavyo si kitu? Maana bila shaka mali hujifanyia mabawa, kama tai arukaye mbinguni.”—Mithali 23:4, 5.
-
-
Dhihirisha Itibari Katika Yehova kwa Kuzoea Mambo UliyojifunzaMnara wa Mlinzi—1988 | Agosti 15
-
-
13. Kwa nini jambo bora zaidi ni kutosheka na “chakula na nguo”?
13 Wale wanaoitibari katika Yehova awaandalie riziki wanajiepushia maumivu na wasiwasi mwingi kwa kufanya hivyo. Ni kweli, kutosheka na “chakula na nguo” tu huenda kukamaanisha kuwa na kiwango cha maisha yaliyo ya kiasi zaidi. (1 Timotheo 6:8) Lakini “vitu vyenye kuthamanika havitakuwa na manufaa yo yote katika ile siku ya kiruu.” (Mithali 11:4, NW) Zaidi ya hilo, wakati sisi tunapoongeza utumishi wetu kwa Yehova, tunajitia katika mstari wa kupata ile “baraka ya Yehova” ambayo “hutajirisha, na yeye haongezi umivu lo lote pamoja nayo.”—Mithali 10:22, NW.
-