-
Je, Yesu Alikuwa Akizungumza Kuhusu Moto wa Mateso?Mnara wa Mlinzi—2008 | Juni 15
-
-
WATU fulani ambao wanaamini fundisho la moto wa mateso wanataja maneno ya Yesu kwenye Marko 9:48 (au mistari 44, 46). Alitaja wadudu (au funza) ambao hawafi na moto ambao hauzimwi. Ikiwa mtu fulani angekuuliza maana ya maneno hayo, ungemwambia nini?
Ikitegemea tafsiri ya Biblia anayotumia, mtu huyo anaweza kusoma mstari wa 44, 46, au 48 kwa sababu tafsiri fulani za Biblia zinatumia maneno yaleyale katika mistari hiyo.a Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inasema hivi: “Ikiwa jicho lako linakufanya ukwazike, litupe mbali; ni afadhali uingie katika ufalme wa Mungu ukiwa na jicho moja kuliko kutupwa katika Gehena ukiwa na macho mawili, mahali ambapo funza wake hafi na ule moto hauzimwi.”—Marko 9:47, 48.
-
-
Je, Yesu Alikuwa Akizungumza Kuhusu Moto wa Mateso?Mnara wa Mlinzi—2008 | Juni 15
-
-
a Hati za Biblia zinazotegemeka zaidi hazina mistari ya 44 na 46. Wasomi wanasema kwamba huenda mistari hiyo miwili iliongezwa baadaye. Profesa Archibald T. Robertson anaandika hivi: “Mistari hiyo miwili haipatikani katika hati bora zaidi na za kale zaidi. Ilitokana na vikundi vya hati za Magharibi na Siria (Bizantiamu). Mistari hiyo inarudia tu mstari wa 48. Kwa hiyo, tunaondoa mistari ya 44 na 46 ambayo si sahihi.”
-