-
Mabadiliko Katika Hali ya Tajiri na LazaroYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Yesu anasema: “Kulikuwa na tajiri ambaye alikuwa akivaa mavazi ya zambarau na kitani, na alifurahia maisha ya kifahari siku kwa siku. Lakini mtu fulani aliyekuwa akiombaomba aliyeitwa Lazaro, alikuwa akiletwa kwenye lango lake. Alikuwa na vidonda mwili mzima, naye alikuwa akitamani kula mabaki yaliyoanguka kutoka kwenye meza ya yule tajiri. Ndiyo, pia, mbwa walikuwa wakija na kuramba vidonda vyake.”—Luka 16:19-21.
-
-
Mabadiliko Katika Hali ya Tajiri na LazaroYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Viongozi hao matajiri wenye kiburi wanawaonaje watu wa kawaida walio maskini? Kwa dharau wanawaona kuwa am ha·’aʹrets, au watu wa nchi (dunia), ambao hawajui Sheria wala hawastahili kufundishwa Sheria. (Yohana 7:49) Hilo linaonyesha hali ya ‘maskini aliyeitwa Lazaro,’ ambaye anatamani “kula mabaki yaliyoanguka kutoka kwenye meza ya yule tajiri.” Kama Lazaro aliyejaa vidonda, watu wa kawaida wanadharauliwa, kana kwamba ni wagonjwa kiroho.
-