-
Yehova Anawapa “Roho Takatifu Wale Wanaomwomba”Mnara wa Mlinzi—2006 | Desemba 15
-
-
5. Mfano wa yule mtu anayeomba bila kuacha unatufundisha nini kuhusu mtazamo wetu tunaposali?
5 Mfano huo ulio wazi wa mtu asiyeacha kuomba unaonyesha mtazamo tunaopaswa kuwa nao tunaposali. Ona kwamba Yesu alisema kuwa mtu huyo anapata anachohitaji “kwa sababu ya kudumu kwake kwa ujasiri.” (Luka 11:8) Maneno ‘kudumu kwa ujasiri’ yanapatikana mara moja tu katika Biblia. Yametafsiriwa kutokana na neno la Kigiriki linalomaanisha kihalisi “kutoona haya.” Mara nyingi, kutoona haya ni sifa mbaya. Hata hivyo, mtu anapoendelea kuomba kitu kizuri bila kuacha au bila kuona haya, sifa hiyo inakuwa nzuri. Ndivyo alivyo yule mtu anayepata mgeni katika mfano huo. Haoni haya kuomba bila kuacha kile anachohitaji. Kwa kuwa Yesu anamtumia mtu huyo kama mfano kwetu, tunapaswa vivyo hivyo kusali bila kuacha. Yehova anataka ‘tuendelee kuomba, tuendelee kutafuta, tuendelee kupiga hodi.’ Na Yehova, ‘atawapa roho takatifu wale wanaomwomba.’
-
-
Yehova Anawapa “Roho Takatifu Wale Wanaomwomba”Mnara wa Mlinzi—2006 | Desemba 15
-
-
9, 10. (a) Toa mfano ambao unaonyesha kwa nini tunahitaji kuendelea kumwomba Mungu roho yake. (b) Tunapaswa kujiuliza swali gani, na kwa nini?
9 Ili kuona jinsi mfano huo unavyotuhusu leo, wazia kwamba mtu fulani katika familia yenu anakuwa mgonjwa katikati ya usiku. Je, ungemwamsha daktari na kumwomba akusaidie? Hungefanya hivyo ikiwa mtu huyo si mgonjwa sana. Hata hivyo, ikiwa angekuwa na mshtuko wa moyo, hungeona haya kumwamsha daktari. Kwa nini? Kwa sababu unakabili hali ya hatari. Unatambua kwamba ni lazima upate msaada wa daktari. Mtu huyo anaweza kufa usipoomba msaada. Vivyo hivyo, Wakristo wa kweli wanaendelea kukabili hali ya hatari. Kwa kweli, Shetani anazunguka-zunguka kama “simba anayenguruma,” akijaribu kutumeza. (1 Petro 5:8) Ili tuendelee kuwa hai kiroho, ni lazima kabisa tupate msaada wa roho ya Mungu. Tusipomwomba Mungu msaada, tunaweza kupata msiba. Hivyo, kwa ujasiri tunaendelea bila kuacha kumwomba Mungu atupe roho yake takatifu. (Waefeso 3:14-16) Ni kwa kufanya hivyo tu ndipo tutaendelea kuwa na nguvu zinazohitajiwa ili ‘kuvumilia mpaka mwisho.’—Mathayo 10:22; 24:13.
-