Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Nisikilizeni Ninapojitetea”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • 17 Baadhi ya wale waliokuwa wamesimama hapo wakashangazwa—si na yule aliyempiga Paulo, bali na jibu la Paulo! Wakamuuliza: “Je, unamtukana kuhani mkuu wa Mungu?” Jibu la Paulo lilionyesha kwamba yeye ni mnyenyekevu na pia anaiheshimu Sheria. Alisema: “Akina ndugu, sikujua yeye ni kuhani mkuu. Kwa maana imeandikwa, ‘Usiseme vibaya juu ya mtawala wa watu wako.’”d (Mdo. 23:4, 5; Kut. 22:28) Paulo akabadili njia yake. Akijua kwamba washiriki wa mahakama hiyo ni Mafarisayo na Masadukayo, akasema: “Wanaume, akina ndugu, mimi ni Farisayo, mwana wa Mafarisayo. Ninahukumiwa kwa sababu ya tumaini la ufufuo wa wafu.”​—Mdo. 23:6.

      Kasisi akiangalia kwa makini andiko katika Biblia yake huku ndugu akimhubiria.

      Kama Paulo alivyofanya, sisi hujaribu kuweka msingi mzuri wa mazungumzo tunapozungumza na watu wenye imani tofauti

      18. Kwa nini Paulo alijiita Farisayo, nasi tunaweza kufuata mfano wake jinsi gani?

      18 Kwa nini Paulo anajiita Farisayo? Kwa sababu alikuwa “mwana wa Mafarisayo” kutoka katika familia ya Kifarisayo. Kwa hiyo, machoni pa wengi alionwa kuwa Farisayo.e Hata hivyo, je, imani ya Paulo kuhusu ufufuo ilikuwa sawa na ya Mafarisayo? Mafarisayo waliamini nafsi haifi, na kwamba nafsi ya waadilifu huishi tena katika miili ya binadamu. Bila shaka, Paulo hakuamini hivyo bali aliamini ufufuo uliofundishwa na Yesu. (Yoh. 5:25-29) Hata hivyo, sawa na Mafarisayo, Paulo aliamini kwamba kuna tumaini la ufufuo. Kwa upande mwingine, Masadukayo hawakuamini kuna ufufuo. Tunaweza kufuata mfano wake tunapowahubiria Wakatoliki au Waprotestanti. Tunaweza kuwaambia sisi pia tunaamini kuna Mungu. Ingawa wanaamini Utatu, sisi tunamwamini Mungu anayetajwa katika Biblia. Hivyo, sote tunaamini kwamba kuna Mungu.

  • “Nisikilizeni Ninapojitetea”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • e Mwaka wa 49 W.K., mitume na wazee walipokuwa wakijadiliana ikiwa Watu wa Mataifa wanapaswa kushika Sheria ya Musa, baadhi ya Wakristo waliokuwako waliitwa “baadhi ya wale wa madhehebu ya Mafarisayo ambao sasa walikuwa waamini.” (Mdo. 15:5) Inaonekana kwa kiasi fulani waamini hao walikuwa bado wakihusianishwa na asili yao ya Kifarisayo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki