-
Paulo Ashinda JangaMnara wa Mlinzi—1999 | Mei 1
-
-
Usiku wa 14 wa dhoruba hiyo, mabaharia wanafanya uvumbuzi wenye kushtusha—kina cha maji ni pima 20 tu.a Baada ya umbali mfupi, wanapima kina tena. Wakati huu maji yana kina cha pima 15. Nchi kavu iko karibu! Lakini habari hizi njema zadokeza jambo lenye kuamsha fikira. Kwa kuwa wanarushwa huku na huku usiku katika maji yenye kina kifupi, meli inaweza kugonga miamba na kuharibika. Kwa hekima, mabaharia wanatia nanga. Baadhi yao wanataka kuteremsha mashua ndogo na kuipanda, wakihatarisha maisha yao baharini.b Lakini Paulo anawazuia. Anawaambia ofisa-jeshi pamoja na askari-jeshi hivi: “Isipokuwa watu hawa wabaki katika mashua, nyinyi hamwezi kuokolewa.” Ofisa huyo anamsikiliza Paulo, na sasa abiria wote 276 wanangojea mapambazuko kwa wasiwasi.—Matendo 27:27-32.
-
-
Paulo Ashinda JangaMnara wa Mlinzi—1999 | Mei 1
-
-
b Mashua ndogo ilitumiwa kwenda ufukoni wakati meli ilipotia nanga karibu na pwani. Kwa wazi, mabaharia walikuwa wakijaribu kuokoa maisha yao huku wakipuuza maisha ya wale wasiokuwa na ustadi wa kuendesha meli, ambao wangeachwa nyuma.
-