-
“Watu Wasio na Elimu na wa Kawaida Tu”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
1, 2. Petro na Yohana walifanya muujiza gani karibu na lango la hekalu?
JUA la alasiri laangaza huku umati ukisongamana. Wayahudi wenye kumwogopa Mungu na wanafunzi wa Yesu wanamiminika kuingia katika ua wa hekalu. “Saa ya sala” inakaribia.a (Mdo. 2:46; 3:1) Wakiwa kati ya umati huo, Petro na Yohana wanaingia kuelekea lango la hekalu lililoitwa Lango Zuri. Katikati ya kelele za umati huo na vishindo vya miguu, mwombaji mwenye umri wa zaidi ya miaka 40, aliyezaliwa akiwa kilema, anaomba zawadi za rehema.—Mdo. 3:2; 4:22.
-
-
“Watu Wasio na Elimu na wa Kawaida Tu”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
a Katika hekalu, sala zilikuwa zikitolewa wakati wa dhabihu za asubuhi na za jioni. Dhabihu ya jioni ilikuwa ikitolewa “saa tisa,” au karibu saa 9 alasiri.
-