Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Nyakati za Kurudishwa” Zimekaribia!
    Mnara wa Mlinzi—2000 | Septemba 1
    • MGAWO huo haungeweza kutimizwa kwa muda wa siku, majuma, au miezi michache. Hata hivyo, wanafunzi hao walianza kuhubiri bila kusita hata kidogo. Lakini hawakuacha kupendezwa na habari iliyohusu kurudishwa. Mtume Petro aliongea na umati mkubwa uliokusanyika Yerusalemu juu ya kurudishwa, akisema: “Tubuni na mgeuke kabisa ili mpate kufutiwa dhambi zenu, ili majira ya kuburudisha yapate kuja kutoka kwa utu wa Yehova na kwamba apate kumtuma Kristo aliyewekwa rasmi kwa ajili yenu, Yesu, ambaye mbingu, kwa kweli, lazima imweke ndani yayo yenyewe hadi nyakati za kurudishwa kwa mambo yote ambayo Mungu alisema kupitia kinywa cha manabii wake watakatifu wa wakati wa kale.”—Matendo 3:19-21.

      Hizo “nyakati za kurudishwa” zingeleta “majira ya kuburudisha” kutoka kwa Yehova. Kurudishwa huko kulikotabiriwa kungefanyika katika hatua mbili. Kwanza, kungekuwa na kurudishwa kwa kiroho kwenye kuburudisha, ambako sasa kunaendelea. Pili, kungefuatwa na kusimamishwa kwa paradiso halisi duniani.

  • “Nyakati za Kurudishwa” Zimekaribia!
    Mnara wa Mlinzi—2000 | Septemba 1
    • Kampeni kubwa ilianzishwa ya kufundisha watu wa mataifa yote washike mambo ambayo Kristo alikuwa amewaamuru wafuasi wake wafanye. (Mathayo 28:20) Iliburudisha kama nini kuona wengine waliokuwa hapo kwanza wameonyesha tabia za kinyama wakibadili mtazamo wao! Walivua kabisa utu wa zamani, ambao hutokeza tabia kama vile “hasira,” “usemi wenye kuudhi,” na “maongezi yenye aibu,” wakavaa utu mpya, “ambao kupitia ujuzi sahihi unafanywa kuwa mpya kulingana na mfano wa [Mungu] aliyeuumba.” Katika maana ya kiroho, maneno ya nabii Isaya yanatimizwa hata sasa: “Mbwa-mwitu [mtu ambaye hapo kwanza alionyesha tabia kama za mbwa-mwitu] atakaa pamoja na mwana-kondoo [mtu aonyeshaye mwelekeo wa upole], na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi; ndama na mwana-simba na kinono watakuwa pamoja.”—Wakolosai 3:8-10; Isaya 11:6, 9.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki