Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yubile ya Kikristo Yafikia Upeo Katika Mileani
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Januari 1
    • 10. Kwa sababu gani tunaweza kutazamia kwamba ukombozi wa ziada na ulio mkubwa zaidi utaonwa na watu?

      10 Ijapokuwa hivyo, kumbuka kwamba katika karne ya kwanza ukomboaji mwingine zaidi ulianza katika Pentekoste 33 W.K. Huko Yubile ya Kikristo ilianza kwa ajili ya “kundi dogo” ambao wangesamehewa dhambi zao, na jambo hilo liwaongoze kuwa “wana wa Mungu” mbinguni. Namna gani katika wakati wetu? Je! mamilioni ya Wakristo wengine wenye kujitoa wangefunguliwa watoke katika kifungo cha dhambi na hivyo washerehekee Yubile kuu? Ndiyo, na mtume Petro alionyesha hivyo aliposema juu ya “zamani za kufanya upya vitu vyote, zilizonenwa na Mungu kwa kinywa cha manabii wake watakatifu [wa kale].”—Matendo 3:21.

  • Yubile ya Kikristo Yafikia Upeo Katika Mileani
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Januari 1
    • 12. Tangu 1935 ni tukio gani lenye kufurahisha ambalo limekuwa likiendelea?

      12 Tangu 1935 “mchungaji mwema” Yesu Kristo amewaingiza wale wanaotaka kuwa: “kondoo wengine” ndani ya ushirika wenye utendaji pamoja na mabaki wapakwa-mafuta Ilikuwa lazima ‘awalete’ hao, nao walipaswa kuwa “kundi moja” chini ya “mchungaji mmoja.” (Yohana 10:16) Sasa “kondoo wengine” ni mamilioni. Ikiwa wewe ni wa umati huo wenye furaha, tayari unahesabiwa kuwa mwadilifu ukiwa rafiki ya Mungu. na ukiwa sehemu ya uumbaji wa kibinadamu unaotazamia ‘kuwekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu’ wakati wa “zamani [zinazokuja] za kufanywa upya vitu vyote” duniani. Hilo si tumaini lililowekwa pasipofaa.—Warumi 8:19-21; Matendo 3:20, 21.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki