Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Biblia Ni Ujumbe Kutoka kwa Mungu
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 6. Kitabu kwa ajili ya watu wote

      Biblia ndicho kitabu ambacho kimetafsiriwa na kusambazwa zaidi duniani. Soma Matendo 10:34, 35, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Kwa nini Mungu anataka Neno lake litafsiriwe na kusambazwa kwa wingi?

      • Wewe binafsi unapendezwa na jambo gani kuhusu Biblia?

      Watu wa jamii na mataifa mbalimbali wakisoma Biblia katika lugha zao.

      Karibu

      Asilimia 100

      ya watu ulimwenguni

      wanaweza kuipata Biblia katika lugha wanayoielewa

      Inapatikana katika lugha zaidi ya

      3,000

      ikiwa nzima

      au sehemu fulani ya Biblia

      5,000,000,000

      Inakadiriwa nakala bilioni tano zimechapishwa,

      idadi kubwa kuliko kitabu kingine chochote

  • Unaweza Kuwa Rafiki ya Yehova
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 3. Yehova anatarajia rafiki zake wafanye nini?

      Yehova anawapenda watu wote, “lakini ana urafiki wa karibu na watu wanyoofu.” (Methali 3:32) Yehova anatarajia rafiki zake wafanye mambo anayoona kuwa mazuri na waepuke mambo mabaya. Baadhi ya watu hufikiri kwamba hawawezi kufuata kikamili viwango vya Yehova kuhusu mema na mabaya. Hata hivyo, Yehova anatuelewa vizuri. Anamkubali kila mtu anayempenda kikweli na anayefanya yote anayoweza ili kumfurahisha.​—Zaburi 147:11; Matendo 10:34, 35.

  • Dumisha Umoja Katika Kutaniko
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 4. Epuka ubaguzi

      Tunapaswa kuwapenda ndugu zetu wote. Lakini huenda ikawa vigumu kushirikiana na mtu ambaye tunamwona kuwa tofauti. Ni nini kitakachotusaidia? Soma Matendo 10:34, 35, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Yehova anakubali watu wa kila aina wawe Mashahidi wake. Unawezaje kuwa na maoni kama ya Yehova kuhusu watu walio na malezi tofauti na yako?

      • Ni ubaguzi wa aina gani ulio katika eneo lenu ambao ungependa kuepuka?

      Soma 2 Wakorintho 6:11-13, kisha mzungumzie swali hili:

      • Unawezaje kuimarisha upendo kati yako na ndugu na dada walio na malezi tofauti na yako?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki