-
Biblia Ni Ujumbe Kutoka kwa MunguFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
6. Kitabu kwa ajili ya watu wote
Biblia ndicho kitabu ambacho kimetafsiriwa na kusambazwa zaidi duniani. Soma Matendo 10:34, 35, kisha mzungumzie maswali haya:
Kwa nini Mungu anataka Neno lake litafsiriwe na kusambazwa kwa wingi?
Wewe binafsi unapendezwa na jambo gani kuhusu Biblia?
Karibu
Asilimia 100
ya watu ulimwenguni
wanaweza kuipata Biblia katika lugha wanayoielewa
Inapatikana katika lugha zaidi ya
3,000
ikiwa nzima
au sehemu fulani ya Biblia
5,000,000,000
Inakadiriwa nakala bilioni tano zimechapishwa,
idadi kubwa kuliko kitabu kingine chochote
-
-
Unaweza Kuwa Rafiki ya YehovaFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
3. Yehova anatarajia rafiki zake wafanye nini?
Yehova anawapenda watu wote, “lakini ana urafiki wa karibu na watu wanyoofu.” (Methali 3:32) Yehova anatarajia rafiki zake wafanye mambo anayoona kuwa mazuri na waepuke mambo mabaya. Baadhi ya watu hufikiri kwamba hawawezi kufuata kikamili viwango vya Yehova kuhusu mema na mabaya. Hata hivyo, Yehova anatuelewa vizuri. Anamkubali kila mtu anayempenda kikweli na anayefanya yote anayoweza ili kumfurahisha.—Zaburi 147:11; Matendo 10:34, 35.
-
-
Dumisha Umoja Katika KutanikoFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
4. Epuka ubaguzi
Tunapaswa kuwapenda ndugu zetu wote. Lakini huenda ikawa vigumu kushirikiana na mtu ambaye tunamwona kuwa tofauti. Ni nini kitakachotusaidia? Soma Matendo 10:34, 35, kisha mzungumzie maswali haya:
Yehova anakubali watu wa kila aina wawe Mashahidi wake. Unawezaje kuwa na maoni kama ya Yehova kuhusu watu walio na malezi tofauti na yako?
Ni ubaguzi wa aina gani ulio katika eneo lenu ambao ungependa kuepuka?
Soma 2 Wakorintho 6:11-13, kisha mzungumzie swali hili:
Unawezaje kuimarisha upendo kati yako na ndugu na dada walio na malezi tofauti na yako?
-