-
“Kujawa na Shangwe na Roho Takatifu”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
1, 2. Safari ya Barnaba na Sauli ina tofauti gani na zile safari nyingine za umishonari, na safari hiyo itasaidiaje kutimiza andiko la Matendo 1:8?
NI SIKU ya shangwe sana katika kutaniko la Antiokia. Kati ya manabii na walimu wote, Barnaba na Sauli ndio waliochaguliwa na roho takatifu kwenda kutangaza habari njema katika sehemu za mbali.a (Mdo. 13:1, 2) Ni kweli kwamba wanaume wanaostahili walitumwa wakati uliopita. Hata hivyo, wakati huo wamishonari hao walienda maeneo ambayo Ukristo ulikuwa umetia mizizi. (Mdo. 8:14; 11:22) Sasa, Barnaba na Sauli—pamoja na Yohana Marko, atakayewahudumia—wanatumwa nchi ambazo watu wengi hawajasikia kamwe habari njema.
2 Miaka 14 hivi iliyopita, Yesu aliwaambia wafuasi wake: “Mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika Yudea yote na Samaria, na mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.” (Mdo. 1:8) Kuwekwa rasmi kwa Barnaba na Sauli kuwa wamishonari kutachangia sana kutimizwa kwa unabii huo wa Yesu!b
-
-
“Kujawa na Shangwe na Roho Takatifu”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
4. (a) Barnaba na Sauli walichaguliwaje, na waabudu wenzao waliitikiaje? (b) Tunawezaje kuwaunga mkono wale wanaopewa mapendeleo ya kitheokrasi?
4 Lakini, kwa nini roho takatifu iliagiza moja kwa moja Barnaba na Sauli wawekwe kando ‘kwa ajili ya kazi’? (Mdo. 13:2) Biblia haisemi. Hata hivyo, tunajua kwamba roho takatifu ilielekeza wanaume hao wachaguliwe. Hatusomi popote kwamba manabii na walimu huko Antiokia walipinga uamuzi huo bali waliunga mkono kabisa uamuzi huo. Wazia jinsi Barnaba na Sauli walivyohisi wakati ndugu zao wa kiroho bila wivu wowote ‘walipofunga na kusali na kuweka mikono juu yao, na kuwaacha waende.’ (Mdo. 13:3) Sisi pia, tunapaswa kuwaunga mkono wale wanaopata mapendeleo ya kitheokrasi, kutia ndani wanaume wanaowekwa rasmi kuwa waangalizi katika kutaniko. Badala ya kuwaonea wivu, tunapaswa ‘kuwafikiria kwa njia inayozidi ile ya kawaida katika upendo kwa sababu ya kazi yao.’—1 The. 5:13.
-