-
Yehova Ana Sifa Gani?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
3. Yehova ameonyeshaje kwamba anatupenda?
Sifa kuu zaidi ya Yehova ni upendo. Na kwa kweli, “Mungu ni upendo.” (1 Yohana 4:8) Yehova amefunua upendo wake kupitia Biblia na vilevile kupitia vitu alivyoumba. (Soma Matendo 14:17.) Kwa mfano, fikiria jinsi alivyotuumba. Ametupatia uwezo wa kuona rangi maridadi, kusikiliza muziki mzuri, na kufurahia chakula kitamu. Anataka tufurahie maisha.
-
-
Thamini Zawadi ya UhaiFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
1. Kwa nini tunapaswa kuuthamini uhai?
Tunapaswa kuuthamini uhai kwa sababu ni zawadi kutoka kwa Baba yetu mwenye upendo, Yehova. Yeye “ndiye chanzo cha uhai,” yaani, aliumba kila kitu kilicho hai. (Zaburi 36:9) “Yeye mwenyewe huwapa watu wote uhai na pumzi na vitu vyote.” (Matendo 17:25, 28) Yehova anatupatia vitu tunavyohitaji ili kuendelea kuwa hai. Zaidi ya hilo, amehakikisha kwamba tunaweza kufurahia maisha.—Soma Matendo 14:17.
-