Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Anaijaza ‘Mioyo Yetu Kikamili’
    Mnara wa Mlinzi—2013 | Julai 1
    • MKARIBIE MUNGU

      Anaijaza ‘Mioyo Yetu Kikamili’

      Je, kweli Mungu anatujali, au je, anaona mateso yanayowapata wanadamu? Biblia inajibu swali hilo kwa njia yenye kuridhisha. Bila shaka, Mungu anawajali wanadamu, na anataka wafurahie maisha. Kila siku anawaruhusu wanadamu kutia ndani wale wasio na shukrani wafaidike na wema wake mwingi. Acheni tuchunguze maneno ya mtume Paulo.​—Soma Matendo 14:16, 17.

      Alipokuwa akihutubia watu wa jiji la Listra ambao hawakuwa waabudu wa Mungu, Paulo alisema hivi: “Katika vizazi vilivyopita [Mungu] aliwaruhusu mataifa yote waendelee kutembea katika njia zao, ijapokuwa, kwa kweli, hakujiacha mwenyewe bila ushahidi kwa kuwa alitenda mema, akiwapa ninyi mvua kutoka mbinguni na majira yenye kuzaa matunda, akijaza mioyo yenu kikamili kwa chakula na uchangamfu.” Maneno hayo yalimaanisha nini kwa wasikilizaji wa Paulo?

      Haikuwa vigumu kwa wakaaji wa Listra kuelewa maneno hayo ya Paulo. Walikuwa wakulima walioishi katika eneo lenye udongo wenye rutuba na maji ya kutosha. Hata hivyo, kama Paulo alivyowakumbusha, Mungu ndiye chanzo cha mvua na majira yenye kuzaa. Kwa hiyo, kila mara walipovuna mazao kwa wingi na kufurahia chakula kitamu, walikuwa wakifaidika na wema wa Mungu.

      Maneno ya Paulo kwa wakaaji wa Listra yanatufundisha masomo muhimu kumhusu Yehova Mungu.

  • Anaijaza ‘Mioyo Yetu Kikamili’
    Mnara wa Mlinzi—2013 | Julai 1
    • Yehova anataka tumjue. Hakujiacha “mwenyewe bila ushahidi,” akasema Paulo. Kitabu cha marejezo kilichotajwa kinasema maneno hayo yanaweza pia kumaanisha “amewaonyesha watu waziwazi yeye ni Mungu wa aina gani.” Uumbaji wa Mungu unaonyesha wazi “sifa zake ambazo hazionekani” kutia ndani wema, hekima, nguvu, na upendo wake. (Waroma 1:20) Yehova amefunua mengi kujihusu katika Biblia. (2 Timotheo 3:16, 17) Je, si ni kweli kwamba anataka tumjue?

      Yehova anataka tuwe na furaha. Anaijaza “mioyo yetu kikamili kwa chakula na uchangamfu,” akasema Paulo. Hata mtenda-dhambi asiyemtambua Yehova anaweza kula na kushiba na kufurahia maisha kwa kadiri fulani. Hata hivyo, Mungu anataka tupate furaha ya kweli na inayodumu. Hilo linawezekana ikiwa tutajifunza ukweli kumhusu na kuutumia maishani.​—Zaburi 144:15; Mathayo 5:3.

      Sote hufaidika kutokana na wema wa Yehova kila siku. Tunakutia moyo ujifunze mengi kuhusu jinsi unavyoweza kuonyesha uthamini kwa Mungu anayejaza moyo wako “kikamili kwa chakula na uchangamfu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki