-
“Akajadiliana Nao Akitumia Maandiko”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
‘Walitaka Paulo na Sila waletwe nje kwenye kile kikundi.’—Matendo 17:5
10 Luka anatueleza kilichofuata: “Wayahudi wakawa na wivu, wakakusanya wanaume fulani waovu waliokuwa wakizurura sokoni, wakafanyiza kikundi chenye ghasia kisha wakazusha fujo jijini. Wakaishambulia nyumba ya Yasoni wakitaka Paulo na Sila waletwe nje kwenye kile kikundi. Walipowakosa wakamkokota Yasoni na baadhi ya akina ndugu mpaka kwa watawala wa jiji, wakisema kwa sauti kubwa: ‘Watu hawa ambao wameipindua dunia inayokaliwa wako hapa pia, naye Yasoni amewakaribisha. Watu hao wote wanapinga maagizo ya Kaisari, wakisema kuna mfalme mwingine, Yesu.’” (Mdo. 17:5-7) Mashambulizi hayo yangewaathirije Paulo na wenzake?
11. Paulo na wenzake walishtakiwa kwa makosa gani, na huenda waliowashtaki walidai wamevunja amri gani? (Ona maelezo ya chini)
11 Kikundi chenye ghasia ni kama mto uliovunja kingo zake, wenye nguvu nyingi na usiozuilika. Wayahudi walitumia kikundi hicho ili kujaribu kuwafukuza Paulo na Sila. Baada ya “kuzusha fujo jijini,” wakajaribu kuwasadikisha watawala kwamba mashtaka yao yalikuwa mazito. Shtaka la kwanza lilikuwa kwamba Paulo na wenzake “wameipindua dunia inayokaliwa,” ingawa Paulo na wenzake hawakusababisha fujo jijini Thesalonike! Shtaka la pili lilikuwa zito zaidi. Wayahudi walidai kwamba wamishonari hao wanamtangaza Mfalme mwingine, Yesu, na hivyo wanavunja sheria ya maliki.a
12. Ni nini kinachoonyesha kwamba mashtaka dhidi ya Wakristo jijini Thesalonike yangeweza kuwa na matokeo mabaya?
12 Kumbuka kwamba viongozi wa kidini walimshtaki Yesu kwa madai yanayofanana na hayo. Walimwambia Pilato: “Tulimkuta mtu huyu akipindua taifa letu . . . akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo mfalme.” (Luka 23:2) Huenda Pilato aliogopa kuwa maliki angefikiri ameachilia kosa kubwa la uhaini, ndio sababu alimhukumu Yesu kwamba anastahili kufa. Vivyo hivyo, mashtaka dhidi ya Wakristo jijini Thesalonike yangekuwa na matokeo mabaya. Kitabu kimoja cha marejeo kinasema: “Mashtaka hayo yalikuwa hatari sana. Ikiwa mtu angetuhumiwa kuwa anataka kumsaliti Maliki, angeweza kuhukumiwa kifo.’” Je, mashtaka hayo yenye chuki yangefanikiwa?
-
-
“Akajadiliana Nao Akitumia Maandiko”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
a Kulingana na msomi mmoja, wakati huo kulikuwa na sheria ya Kaisari iliyokataza utabiri wowote kuhusu “kuja kwa mfalme au ufalme mpya, hasa mfalme anayeweza kumwondoa au kumhukumu maliki anayetawala.” Huenda adui za Paulo walifanya ujumbe wa mtume huyo uonekane kana kwamba unakiuka sheria hiyo. Ona sanduku lenye kichwa “Kaisari Wanaotajwa Katika Kitabu cha Matendo.”
-