Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ubatizo
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
    • Yehova Mungu ndiye mwenye daraka la kufanya ubatizo huo katika Kristo Yesu na vilevile ubatizo katika kifo chake. Alimtia Yesu mafuta, akamfanya kuwa Kristo au Mtiwa Mafuta. (Mdo 10:38) Hivyo, Mungu alimbatiza Yesu kwa roho takatifu ili, kupitia Yesu, baada ya hapo wafuasi wake waweze kubatizwa kwa roho takatifu. Kwa hiyo, wale wanaokuwa warithi wenzi pamoja naye, wakiwa na matumaini ya kimbingu, wanapaswa ‘kubatizwa katika Kristo Yesu,’ yaani, katika Mtiwa Mafuta Yesu ambaye, wakati wa kutiwa mafuta, alizaliwa pia awe mwana wa kiroho wa Mungu. Kwa kufanya hivyo wanaunganishwa pamoja naye, Kichwa chao, nao wanakuwa washiriki wa kutaniko ambalo ni mwili wa Kristo.—1Ko 12:12, 13, 27; Kol 1:18.

  • Mwili
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
    • Matumizi ya Mfano. Yesu Kristo anatajwa akiwa Kichwa cha “kutaniko, ambalo ni mwili wake.” (Efe 1:22, 23; Kol 1:18) Mwili huo wa watu wa Kikristo hauna migawanyiko ya kitabaka, kitaifa, au vinginevyo, Wayahudi na watu wa mataifa yote wakiwakilishwa nao. (Gal 3:28; Efe 2:16; 4:4) Wote wanabatizwa kwa roho takatifu katika Kristo na katika kifo chake. Kwa hiyo, wote wanabatizwa katika mwili mmoja. (1Ko 12:13) Hivyo basi, mwili wote unamfuata kichwa, ukifa katika kifo kama chake na kupokea ufufuo kama wake.​—Ro 6:3-5; ona UBATIZO (Kubatizwa Katika Kristo Yesu, Katika Kifo Chake).

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki