-
Hii Ndiyo Siku ya Wokovu!Mnara wa Mlinzi—1998 | Desemba 15
-
-
12. Ni huduma gani muhimu ambayo inatekelezwa na mabalozi na wajumbe wa Yehova?
12 Ili kupata wokovu, ni lazima tutende kupatana na maneno ya Paulo: “Tukiwa tunafanya kazi pamoja naye [Yehova], twawasihi sana nyinyi pia msiipokee fadhili isiyostahiliwa ya Mungu na kukosa kusudi layo. Kwa maana yeye asema: ‘Wakati wenye kukubalika nilikusikia, na siku ya wokovu nilikusaidia.’ Tazameni! Sasa ndio wakati wenye kukubalika hasa. Tazameni! Sasa ndiyo siku ya wokovu.” (2 Wakorintho 6:1, 2) Mabalozi wa Yehova watiwa-mafuta na wajumbe wake, “kondoo wengine,” hawakubali fadhili isiyostahiliwa ya Baba yao wa kimbingu na kukosa kusudi lake. (Yohana 10:16) Kwa mwenendo wao mwadilifu na huduma yao yenye bidii katika “wakati [huu] wenye kukubalika,” wao wanatafuta upendeleo wa Mungu na wanawaarifu wakazi wa dunia kwamba hii ndiyo “siku ya wokovu.”
13. Jambo kuu katika andiko la Isaya 49:8 ni lipi, nalo lilitimizwaje kwa mara ya kwanza?
13 Paulo anukuu andiko la Isaya 49:8, lisemalo hivi: “BWANA asema hivi, Wakati uliokubalika [“wakati wa nia njema,” NW] nimekujibu, na siku ya wokovu nimekusaidia; nami nitakuhifadhi, nitakutoa uwe agano la watu hawa, ili kuiinua nchi hii, na kuwarithisha urithi uliokuwa ukiwa.” Unabii huo ulitimizwa mara ya kwanza wakati Waisraeli walipowekwa huru na utekwa wa Babiloni na baadaye wakarudi katika nchi yao iliyokuwa ukiwa.—Isaya 49:3, 9.
14. Andiko la Isaya 49:8 lilitimizwaje katika kisa cha Yesu?
14 Katika utimizo zaidi wa unabii wa Isaya, Yehova alimtoa Yesu “mtumishi” wake kuwa ‘nuru ya mataifa, apate kuwa wokovu wa Mungu hata miisho ya dunia.’ (Isaya 49:6, 8; linganisha Isaya 42:1-4, 6, 7; Mathayo 12:18-21.) Kwa wazi, “wakati wa nia njema,” au “wakati wenye kukubalika,” ulitumiwa kumrejezea Yesu alipokuwa duniani. Alisali, na Mungu ‘akamjibu.’ Hiyo ilithibitika kuwa “siku ya wokovu” kwa Yesu kwa sababu alidumisha uaminifu-maadili na hivyo “akawa ndiye mwenye daraka la wokovu udumuo milele kwa wale wote wanaomtii yeye.”—Waebrania 5:7, 9; Yohana 12:27, 28.
15. Tangu lini Waisraeli wa kiroho wamejitahidi kuthibitika kuwa wastahili fadhili ya Mungu isiyostahiliwa, na kwa lengo gani?
15 Paulo atumia andiko la Isaya 49:8 kuwarejezea Wakristo watiwa-mafuta, akiwasihi ‘wasikose kusudi la fadhili isiyostahiliwa ya Mungu’ kwa kushindwa kutafuta nia njema yake katika “wakati wenye kukubalika” na “siku ya wokovu” aandaayo. Paulo aongeza kusema: “Tazameni! Sasa ndio wakati wenye kukubalika hasa. Tazameni! Sasa ndiyo siku ya wokovu.” (2 Wakorintho 6:2) Tangu Pentekoste mwaka wa 33 W.K., Waisraeli wa kiroho wamejitahidi kuthibitika kuwa wastahili fadhili ya Mungu isiyostahiliwa ili “wakati wenye kukubalika” uwe “siku ya wokovu” kwao.
-
-
Hii Ndiyo Siku ya Wokovu!Mnara wa Mlinzi—1998 | Desemba 15
-
-
Tumaini Kuokolewa na Yehova
20. (a) Paulo alitamani nini sana, na kwa nini hakukuwa na wakati wa kupoteza? (b) Ni nini kiashiriacho siku ya wokovu tunamoishi sasa?
20 Paulo alipowaandikia Wakorintho barua yake ya pili wapata mwaka wa 55 W.K., mfumo wa mambo wa Kiyahudi ulikuwa umebakiza miaka 15 hivi. Mtume huyo alitamani sana Wayahudi na Wasio Wayahudi wapatanishwe na Mungu kupitia Kristo. Hiyo ilikuwa siku ya wokovu, na hakukuwa na wakati wa kupoteza. Tangu 1914, sisi tumekuwa katika umalizio wa mfumo wa mambo unaolingana na huo. Kazi ya tufeni pote ya kuhubiri Ufalme inayoendelea sasa yaiashiria hii kuwa siku ya wokovu.
21. (a) Ni andiko gani ambalo limechaguliwa kwa ajili ya mwaka wa 1999? (b) Twapaswa kuwa tukifanya nini katika hii siku ya wokovu?
21 Watu wa mataifa yote wahitaji kujua juu ya uandalizi wa Mungu wa kupata wokovu kupitia Yesu Kristo. Hakuna wakati wa kukawia. Paulo aliandika: “Tazameni! Sasa ndiyo siku ya wokovu.” Maneno hayo ya 2 Wakorintho 6:2 yatakuwa andiko la mwaka wa 1999 la Mashahidi wa Yehova. Lafaa jinsi gani, kwa kuwa twakabili jambo lililo baya zaidi kuliko kuharibiwa kwa Yerusalemu na hekalu lake! Mwisho wa mfumo huu wote wa mambo, unaohusisha kila mtu duniani, uko karibu sana. Sasa—wala si kesho—ndio wakati wa kutenda. Ikiwa twaamini kwamba wokovu ni wa Yehova, ikiwa twampenda, na ikiwa twathamini uhai, hatutakosa kusudi la fadhili isiyostahiliwa ya Mungu. Tukiwa na tamaa yenye kuhisiwa moyoni ya kumstahi Yehova, tutathibitisha kwa neno na tendo kwamba kwa kweli twamaanisha tusemalo, tunaposema hivi kwa mkazo: “Tazameni! Sasa ndiyo siku ya wokovu.”
-