Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Uthamini kwa Ndugu Zetu
    Mnara wa Mlinzi—1988 | Oktoba 1
    • 10 Katika Linguistic Key to the Greek New Testament, Fritz Rienecker anatoa maelezo juu ya neno lililotafsiriwa “kwa juhudi nyingi sana,” au ‘kwa kunyooka kirefurefu,’ katika 1 Petro 1:22. Yeye anaandika hivi: “Wazo la kimsingi ni lile la bidii ya moyoni, ujitahidi (kufanya jambo si kijuujuu . . . bali [kwa] kujikakamua) (Hort).” Miongoni mwa maana nyinginezo, kujikakamua kunamaanisha “kujinyoosha kufikia kiwango cha mwisho.” Kwa hiyo kupendana mmoja na mwenzake kutoka moyoni kunamaanisha kujikaza wenyewe kufikia upeo katika jitihada zetu za kuwa na shauku ya kidugu kwa waandamani wetu wote wa Kikristo. Je! baadhi ya ndugu na dada zetu wamefinyika kwa kukosa kupewa nafasi katika shauku zetu nyororo? Ikiwa ndivyo, inatupasa sisi tupanuke.

  • Uthamini kwa Ndugu Zetu
    Mnara wa Mlinzi—1988 | Oktoba 1
    • 11, 12. (a) Ni shauri gani ambalo mtume Paulo aliwapa Wakristo katika Korintho? (b) Ni jinsi gani Paulo alivyoweka kielelezo kizuri katika habari hiyo?

      11 Inaonekana mtume Paulo alihisi uhitaji wa jambo hilo katika kundi la Korintho. Yeye aliwaandikia hivi Wakristo wa huko: “Kinywa chetu kimefunguliwa kwa ninyi, Wakorintho, moyo yetu umepanuka. Ninyi hamfinyiki kwa kukosa kupewa nafasi ndani yetu, bali ninyi mnafinyika kwa kukosa kupewa nafasi katika shauku nyororo zenu wenyewe. Kwa hiyo, kama kwamba mnafanya malipo ya kurudisha​—mimi nanena kama kwa watoto​—ninyi, pia, panukeni.”​—2 Wakorintho 6:11-13, NW.

      12 Ni jinsi gani sisi tunaweza kupanua mioyo yetu ili itie ndani ndugu na dada zetu wote? Paulo aliweka kielelezo kizuri katika jambo hilo. Kwa uwazi yeye alitafuta kilicho bora zaidi katika ndugu zake, na hakuwakumbuka kwa ajili ya makosa ya kupungukiwa kwao bali kwa ajili ya sifa zao njema. Sura ya kufungia barua yake kwa Wakristo katika Roma inatoa kielezi cha jambo hilo. Acheni tuchunguze Waroma sura ya 16 na kuona jinsi inavyoonyesha mwelekeo chanya wa Paulo kuhusu ndugu na dada zake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki