Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Agano la Mungu Pamoja na “Rafiki” Yake Tayari Lafaidi Mamilioni
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
    • 11. Mtume Paulo alielezaje jambo lililotukia kwa wazao wa asili wa Abrahamu?

      11 Mtume Paulo anatuelezea jambo hilo akisema: “Imeandikwa kwamba Abrahamu alipata wana wawili, yule mmoja kwa yule msichana-mtumishi [Hagari] na mmoja kwa yule mwanamke aliye huru [Sara]; lakini yule mmoja kwa msichana-mtumishi kwa kweli alizaliwa kwa jinsi ya mwili, yule mwingine kwa yule mwanamke aliye huru kupitia ahadi. Mambo haya yanakuwa kama mchezo wa kuigiza; kwa kuwa wanawake hawa wanafananisha maagano mawili, lile moja katika Mlima Sinai, ambalo linazaa watoto kwa utumwa, na ndilo Hagari. Basi huyu Hagari anamaanisha Sinai, Mlima katika Uarabu, naye analingana na Yerusalemu leo, kwa kuwa yumo katika utumwa pamoja na watoto wao. Lakini Yerusalemu wa juu yuko huru, naye ni mama yetu sisi.”—Wagalatia 4:22-26, NW.

  • Agano la Mungu Pamoja na “Rafiki” Yake Tayari Lafaidi Mamilioni
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
    • 13. (a) Ni nini kilicholingana na Sara, mke wa Abrahamu? (b) Kwa sababu gani “Yerusalemu wa juu” unaweza kuitwa “huru”?

      13 Kwa upande mwingine, “Yerusalemu wa juu” ulikuwa tengenezo lisiloonekana la kimbingu la Yehova. Kwa kulingana, lingeweza kufananishwa na mwanamke, na Sara, yule mke wa kweli wa Abrahamu. Lile agano la torati halikufanywa pamoja na tengenezo hilo, kwa hiyo “Yerusalemu wa juu” alikuwa huru, kama Sara wa kale. Hilo ndilo tengenezo linalotokeza ule “uzao” ulioahidiwa, na ndiyo sababu mtume Paulo angeweza kuliita “mama yetu sisi.”

      14. Je! Agano la Kiabrahamu linahusu “Yerusalemu wa juu,” na kwa hiyo wale wanafunzi wa Yesu Kristo waliozaliwa kwa roho wanaweza kuitwaje?

      14 Kwa kweli, basi, lile agano la Kiabrahamu linamhusu yeye akiwa ndiye mke wa mfano wa Abrahamu Mkubwa Zaidi, ndiyo, linahusu tengenezo la Yehova la ulimwengu mzima huko juu mbinguni. Kwa hiyo wale wanafunzi wa Yesu Kristo waliozaliwa kwa roho, kama vile mtume Paulo, ni wana au watoto wa agano la Kiabrahamu. Paulo anaendelea kutoa sababu kwa njia hiyo akisema:

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki