Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Unajitahidi Kukomaa Kiroho?
    Mnara wa Mlinzi—2015 | Septemba 15
    • 2 Vivyo hivyo, Yehova anataka watumishi wake wakomae kiroho. Kwa hiyo baada ya kujiweka wakfu na kubatizwa, Mkristo anapaswa kuwa na lengo la kukomaa kiroho. Mtume Paulo aliwaandikia Wakristo wa Efeso kuhusu uhitaji wa kukua kiroho. Aliwatia moyo wajitahidi kufikia ‘umoja katika imani na ujuzi sahihi wa Mwana wa Mungu, na kuwa watu waliokomaa, kufikia kipimo cha kimo ambacho ni cha ujazo wa Kristo.’—Efe. 4:13.

      3. Hali iliyokuwa katika kutaniko la Efeso inafananaje na hali ya watu wa Yehova leo?

      3 Kutaniko la Efeso lilikuwa limedumu kwa miaka kadhaa tangu lianzishwe wakati Paulo alipoliandikia barua. Wanafunzi wengi kutanikoni walikuwa wamekomaa kiroho. Hata hivyo, baadhi yao walihitaji kujitahidi ili wawe wakomavu. Hali iko hivyo leo miongoni mwa Mashahidi wa Yehova. Ndugu na dada wengi wamemtumikia Mungu kwa miaka mingi, nao wamekomaa kiroho. Lakini ni wazi kwamba si wote wamefikia hatua hiyo. Kwa mfano, maelfu ya watu hubatizwa kila mwaka, hivyo wengine bado wanahitaji kujitahidi kukomaa. Namna gani wewe?—Kol. 2:6, 7.

  • Je, Unajitahidi Kukomaa Kiroho?
    Mnara wa Mlinzi—2015 | Septemba 15
    • 5 Mkristo mkomavu anamwiga Yesu, ambaye alituwekea mfano mzuri ili tufuate “hatua zake kwa ukaribu.” (1 Pet. 2:21) Yesu alikazia jambo gani muhimu zaidi? Alisema kwamba tunapaswa kumpenda Yehova kwa moyo, nafsi, na akili yetu yote na pia kumpenda jirani yetu kama tunavyojipenda wenyewe. (Mt. 22:37-39) Mkristo mkomavu anajitahidi kutii amri hiyo. Maisha yake yanaonyesha kwamba anathamini sana uhusiano wake na Yehova na anawapenda wengine kutoka moyoni.

  • Je, Unajitahidi Kukomaa Kiroho?
    Mnara wa Mlinzi—2015 | Septemba 15
    • 8. Ni nini kinachoonyesha kwamba Yesu aliyaelewa vizuri Maandiko?

      8 Yesu Kristo aliyaelewa vizuri sana Maandiko. Alipokuwa na umri wa miaka 12, alitumia Maandiko kujadiliana na walimu hekaluni. “Wale wote waliokuwa wakimsikiliza walikuwa wakishangazwa daima na uelewaji wake na majibu yake.” (Luka 2:46, 47) Baadaye, wakati wa huduma yake, Yesu aliwanyamazisha adui zake kwa kutumia Neno la Mungu.—Mt. 22:41-46.

      9. (a) Mkristo anayetamani kukua kiroho anapaswa kufanya nini kwa ukawaida? (b) Kwa nini tunajifunza Neno la Mungu?

      9 Mkristo anayetamani kukua kiroho anajitahidi kuiga mfano wa Yesu na haridhiki tu kujua mambo ya msingi. Badala yake anachunguza kwa kina Maandiko, akitambua kwamba “chakula kigumu ni cha watu wakomavu.” (Ebr. 5:14) Bila shaka Mkristo mkomavu ana lengo la kupata “ujuzi sahihi wa Mwana wa Mungu.” (Efe. 4:13) Je, unasoma Biblia kila siku? Je, unajifunza kibinafsi kwa ukawaida, ukijitahidi kutenga wakati kila juma kwa ajili ya ibada ya familia? Unaposoma Neno la Mungu, uwe chonjo kutambua kanuni za Biblia zitakazokusaidia kujua maoni na hisia za Yehova. Kisha, jitahidi kuzitumia maishani kwa kuwa kufanya hivyo kutakusaidia umkaribie zaidi Yehova.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki