Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Endeleeni Kusameheana kwa Hiari’
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Desemba 1
    • 5. Ni sababu gani ya maana ya kusamehe wengine ambayo imeonyeshwa kwenye Waefeso 5:1?

      5 Sababu ya maana ya kuwasamehe wengine yaonyeshwa kwenye Waefeso 5:1: “Kwa hiyo, iweni waigaji wa Mungu, mkiwa watoto wapendwa.” Twapaswa kuwa “waigaji wa Mungu” katika jambo gani? Maneno “kwa hiyo” yaunganisha huo usemi na mstari unaotangulia, ambao wasema hivi: “Iweni wenye fadhili nyinyi kwa nyinyi, wenye huruma kwa njia nyororo, mkisameheana kwa hiari mtu na mwenzake kama vile Mungu pia kupitia Kristo alivyowasamehe nyinyi kwa hiari.” (Waefeso 4:32) Ndiyo, kwa habari ya msamaha, twapaswa kuwa waigaji wa Mungu. Kama vile mvulana mdogo hujaribu kuwa tu kama baba yake, sisi, tukiwa watoto ambao Yehova apenda sana, yatupasa tutake kuwa kama Baba yetu wa kimbingu mwenye kusamehe. Lazima Yehova awe apendezwa kama nini kutazama chini kutoka mbinguni na kuona watoto wake wa kidunia wakijaribu kuwa kama yeye kwa kusameheana!—Luka 6:35, 36; linganisha Mathayo 5:44-48.

      6. Ni katika njia gani kuna tofauti kubwa kati ya msamaha wa Yehova na msamaha wetu?

      6 Ni kweli, hatuwezi kamwe kusamehe kikamilifu kama vile Yehova hufanya. Lakini hiyo ndiyo sababu zaidi twapaswa kusameheana. Fikiria hili: Kuna tofauti kubwa kati ya msamaha wa Yehova na msamaha wetu. (Isaya 55:7-9) Tuwasamehepo wale ambao wamefanya dhambi dhidi yetu, mara nyingi sisi hufanya hivyo kwa kufahamu kwamba huenda siku moja tukahitaji watufanyie vivyo hivyo. Kwa habari ya wanadamu, sikuzote inakuwa hali ya watenda-dhambi kuwasamehe watenda-dhambi. Hata hivyo, kwa habari ya Yehova msamaha ni wa upande mmoja sikuzote. Yeye hutusamehe, lakini hatutahitaji kumsamehe kamwe. Ikiwa Yehova, ambaye hafanyi dhambi, aweza kutusamehe kwa upendo na kwa ukamili hivyo, je, haitupasi sisi wanadamu wenye dhambi kujaribu kusameheana?—Mathayo 6:12.

  • ‘Endeleeni Kusameheana kwa Hiari’
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Desemba 1
    • 11. Wengine wafanyapo dhambi dhidi yetu, ni nini liwezalo kutusaidia tuwasamehe?

      11 Hata hivyo, namna gani ikiwa wengine wafanya dhambi dhidi yetu, wakisababisha jeraha lenye kuonekana? Ikiwa hiyo dhambi si zito mno, huenda tukapata ugumu kidogo wa kutumia shauri la Biblia la ‘kusameheana kwa hiari mtu na mwenzake.’ (Waefeso 4:32) Utayari kama huo wa kusamehe wapatana na maneno haya ya Petro yaliyopuliziwa: “Juu ya mambo yote, iweni na upendo wenye juhudi nyingi nyinyi kwa nyinyi, kwa sababu upendo hufunika wingi wa dhambi.” (1 Petro 4:8) Kukumbuka kwamba sisi pia ni watenda-dhambi hutusaidia kuachilia makosa ya wengine. Tusamehepo hivyo, twaachilia uchungu wa moyo badala ya kuusitawisha. Tokeo ni kwamba, huenda ikawa uhusiano wetu na mkosaji hautapatwa na madhara yoyote ya kudumu, nasi pia twasaidia kuhifadhi amani yenye thamani ya kutaniko. (Waroma 14:19) Halafu, huenda kumbukumbu la jambo alilofanya likafifia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki