Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tumikieni Yehova kwa Upatano Mmoja
    Mnara wa Mlinzi—1988 | Mei 15
    • Fikiria Wengine Kuwa Bora Kuliko Wewe

      11. Ikiwa upendeleo wa aina yo yote umo katika moyo wa Mkristo, yeye anaweza kufanya nini?

      11 Kwa upande ule mwingine, ikiwa Mkristo alikuwa mwenye upendeleo kwa jamii ya watu wa rangi au utaifa mmoja, labda yeye angeonyesha hivyo kwa maneno au vitendo. Hilo nalo lingeweza kusababisha hisia zilizojeruhiwa, hasa katika kundi lenye watu wa malezi ya makabila mbalimbali. Kwa uhakika, hakuna Mkristo ambaye angetaka kuweka mgogoro huo juu ya watu wa Mungu. (Zaburi 133:1-3) Kwa hiyo ikiwa upendeleo wo wote umo katika moyo wa Mkristo, yeye anaweza hata kusali hivi: “Nipekue-pekue mimi ndani ya sehemu zote, O Mungu, na ujue moyo wangu Nichunguze mimi, na ujue fikira zangu zenye kunikosesha utulivu, na uone kama ndani yangu mna njia yo yote yenye umivu, na uniongoze mimi katika njia ya wakati usio dhahiri.”​—⁠Zaburi 139:23, 24, NW.

      12. Kwa sababu gani haitupasi kujisifu wenyewe au kuhusu wengine walio wa malezi ya kabila letu?

      12 Ni vizuri kufuata maoni yale ya kiasi kwamba sisi sote ni wanadamu wasiokamilika ambao wasingaliweza hata kidogo kuwa na msimamo wo wote pamoja na Mungu kama isingalikuwa ni kwa sababu ya dhabihu ya Yesu Kristo. (1 Yohana l:​8–2:2) Ni nini, basi, kinachotufanya tofauti na wengine? Kwa kuwa sisi hatuna cho chote ambacho hatukupokea, mbona sisi tujisifu katika sisi wenyewe au katika wengine walio wa malezi ya kabila letu?​—⁠Linganisha 1 Wakorintho 4:6, 7.

      13. Ni jinsi gani sisi tunaweza kuchangia umoja wa kundi, na tunaweza kujifunza nini kutokana na Wafilipi 2:1-11?

      13 Sisi tunaweza kuchangia umoja wa kundi tukikiri na kuonyesha uthamini kwa sifa njema za wengine. Paulo mtume Myahudi alitupa sisi sote jambo la kufikiria sana alipowaambia hivi Wafilipi Wamataifa: “Fanyeni shangwe yangu iwe kamili katika jambo la kwamba ninyi ni wa akili ile ile moja na mna upendo ule ule mmoja, mkiwa mnaunganishwa pamoja katika nafsi, mkishikilia fikira moja katika akili, bila kufanya lo lote kwa ushindani au kwa majivuno, bali kwa udhalili wa akili mkifikiria kwamba wengine ni bora kuliko ninyi.” Mwelekeo unaofaa sisi tuonyeshe kuelekea wanadamu wenzetu wa jamii ya watu wa rangi au utaifa wo wote ulionyeshwa kwa kielelezo katika Yesu Kristo. Ingawa yeye alikuwa kiumbe-roho mwenye uweza, yeye “alikuja kuwa katika ufanani wa wanadamu” na akajinyenyekeza mwenyewe kufikia kifo juu ya mti wa mateso kwa ajili ya wanadamu wenye dhambi wa kila rangi ya jamii ya watu na taifa. (Wafilipi 2:1-11, NW) Basi, kwa kuwa sisi ni wafuasi wa Yesu, je! haitupasi kuwa wenye upendo, wanyenyekevu, na wenye huruma, tukikiri kwamba wengine ni bora kuliko sisi?

      Sikiliza na Kutazama Sana

      14. Tunaweza kusaidiwa jinsi gani kufikiria wengine kuwa bora kuliko sisi?

      14 Huenda sisi tukasaidiwa kufikiria wengine kuwa bora kuliko sisi tukisikiliza kweli kweli wakati wao wanaponena, na kutazama mwenendo wao kwa uangalifu. Mathalani, huenda tukalazimika kukubali kwa moyo wa kufuata haki kwamba mzee mwenzetu​—⁠labda wa jamii ya watu wa rangi nyingine​—⁠ametupita sisi katika uwezo wa kutoa mashauri yenye matokeo mazuri katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Huenda tukatambua kwamba ni hali yake ya kiroho, si kwa lazima uteuzi wake wa maneno ya ufasaha au njia ya kunena, inayomwezesha apate matokeo mazuri katika kusaidia waitikadi wenzetu wawe watangazaji hodari wa Ufalme. Na ni wazi kwamba Yehova anabariki jitihada zake.

      15. Huenda sisi tukaona nini wakati tunaposikiliza taarifa za waabudu wenzetu?

      15 Wakati sisi tunapoongea na ndugu na dada zetu au kusikiliza maelezo yao kwenye mikutano, huenda tukahisi kwa fahamu zetu kwamba watu fulani kati yao wana ufahamivu mzuri zaidi wa kweli fulani za Kimaandiko kuliko sisi. Huenda tukatambua kwamba upendo wao wa kidugu unaonekana kuwa wenye imara zaidi, wao wanaonekana kuwa wenye imani zaidi, au wanatoa ithibati ya kuitibari zaidi katika Yehova. Kwa hiyo wawe au wasiwe ni wa malezi ya kabila letu, wao wanatuchochea kwenye upendo na kazi nzuri, wanasaidia kuimarisha imani yetu, na wanatusukuma tuitibari kwa ukamili zaidi katika Baba yetu wa kimbingu. (Mithali 3:5, 6; Waebrania 10:24, 25, 39) Kwa uwazi Yehova amejileta awe karibu nao, na inatupasa sisi pia tufanye hivyo.​—⁠Linganisha Yakobo 4:8.

  • Tumikieni Yehova kwa Upatano Mmoja
    Mnara wa Mlinzi—1988 | Mei 15
    • 20. Staha yetu kwa waitikadi wenzetu wa kila rangi ya jamii ya watu na taifa inaweza kuongezwa jinsi gani?

      20 Pasipo swali, Yehova hubariki na kutegemeza mashahidi wake wa kila taifa na rangi ya jamii ya watu. Yeye si mwenye upendeleo na kwa kuwa sisi ni watumishi wake waliojiweka wakfu, sisi hatuna udhuru wala sababu yo yote ya kuonyesha upendeleo. Waaidha, staha yetu kwa ndugu na dada zetu wa kila rangi ya jamii ya watu na taifa itaongezeka tukifikiria njia ambazo wao ni bora kuliko sisi. Wao pia wanatumia hekima ya kimbingu, ambayo haifanyi mipambanuo ya upendeleo bali inazaa tunda bora kabisa. (Yakobo 3:13-18) Ndiyo, na fadhili yao, ukarimu, upendo, na sifa zile nyingine zao za kutii Mungu zinatuandalia vielelezo vizuri sana.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki