-
Watu wa Yehova ‘Hukataa Ukosefu wa Uadilifu’Mnara wa Mlinzi—2014 | Julai 15
-
-
9. “Maswali ya upumbavu na ya kijinga” yaliathirije kutaniko la Kikristo katika karne ya kwanza?
9 Neno la Mungu linatoa shauri hususa kuhusu ukosefu wa uadilifu ambao lazima Wakristo wakatae au kuepuka. Kwa mfano, kabla ya kutaja maneno yaliyo katika 2 Timotheo 2:19, Paulo anamwambia Timotheo ‘asipigane juu ya maneno’ na ‘aepuke kabisa maneno matupu.’ (Soma 2 Timotheo 2:14, 16, 23.) Washiriki fulani wa kutaniko walikuwa wakieneza mafundisho ya uasi-imani. Inaonekana pia kwamba wengine walianzisha mawazo yaliyoleta ubishi. Mawazo hayo yalisababisha migawanyiko hata kama hayakupingana moja kwa moja na maandiko. Yalisababisha ugomvi na mabishano kuhusu maneno, jambo lililohatarisha hali yao ya kiroho. Hivyo, Paulo alikazia umuhimu wa ‘kukataa maswali ya upumbavu na ya kijinga.’
10. Tunapaswa kufanya nini tunapokabili uasi-imani?
10 Siku hizi, si rahisi kupata waasi-imani katika kutaniko la watu wa Yehova. Hata hivyo, ni lazima tukatae kwa uthabiti mafundisho yasiyopatana na Biblia, haidhuru yanatoka katika chanzo gani. Si jambo la hekima kubishana na waasi-imani, iwe ni moja kwa moja au kupitia Intaneti, au kwa kuwasiliana nao kwa njia nyingine yoyote. Kuzungumza na mwasi-imani hata kwa nia ya kumsaidia ni kinyume cha mwongozo wa Maandiko tuliyochunguza. Badala yake, tukiwa watu wa Yehova, tunaepuka na kukataa katakata uasi-imani.
Usibishane na waasi-imani (Tazama fungu la 10)
11. Ni nini kinachoweza kusababisha “maswali ya upumbavu,” na wazee Wakristo wanawezaje kuweka mfano mzuri?
11 Mbali na uasi-imani, kuna mambo mengine yanayoweza kuvuruga amani ya kutaniko. Kwa mfano, maoni yanayotofautiana kuhusu burudani yanaweza kutokeza “maswali ya upumbavu na ya kijinga.” Bila shaka Mkristo anapowachochea wengine kushiriki katika burudani zinazovunja viwango vya Yehova vya maadili, wazee Wakristo hawapaswi kuruhusu tabia hiyo eti kwa sababu hawataki mabishano. (Zab. 11:5; Efe. 5:3-5) Hata hivyo, wazee huwa waangalifu ili wasiwalazimishe wengine kufuata maoni yao. Wanatii kwa ushikamanifu shauri hili la Kimaandiko wanalopewa waangalizi Wakristo: ‘Lichungeni kundi la Mungu lililo chini ya uangalizi wenu, wala si kwa kupiga ubwana juu ya wale ambao ni urithi wa Mungu, bali kuwa vielelezo kwa kundi.’—1 Pet. 5:2, 3; soma 2 Wakorintho 1:24.
-
-
Watu wa Yehova ‘Hukataa Ukosefu wa Uadilifu’Mnara wa Mlinzi—2014 | Julai 15
-
-
13 Kanuni za Biblia tulizochunguza hazihusu tu burudani. Maoni yanayotofautiana kuhusu mavazi na kujipamba, afya na vyakula, na mambo mengine ya kibinafsi yanaweza pia kuchochea mabishano. Hivyo, ikiwa hakuna kanuni yoyote ya Biblia inayovunjwa, watu wa Yehova huepuka kwa busara kubishana kuhusu mambo hayo, kwa sababu ‘mtumwa wa Bwana hahitaji kupigana, bali anahitaji kuwa mpole au mwenye busara kwa wote.’—2 Tim. 2:24.
-