-
Jinsi Dini za Uwongo Zinavyopotosha Ukweli Kumhusu MunguFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
2. Matendo ya dini za uwongo yanapotoshaje ukweli kumhusu Mungu?
Dini za uwongo huwatendea watu kinyume cha mapenzi ya Yehova. Biblia inasema kwamba “dhambi [za dini za uwongo] zimekusanyika pamoja mpaka mbinguni.” (Ufunuo 18:5) Kwa karne nyingi, dini za uwongo zimejihusisha na siasa, zimeunga mkono vita na kusababisha vifo vya watu wengi sana. Baadhi ya viongozi wa dini huishi maisha ya kifahari kwa kuwalazimisha wafuasi wao watoe sadaka. Matendo hayo yanathibitisha kwamba hawamjui Mungu na kwamba hawapaswi kumwakilisha.—Soma 1 Yohana 4:8.
-
-
Endelea Kuwa Mshikamanifu kwa YehovaFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
Soma Luka 4:8 na Ufunuo 18:4, 5, kisha ujibu maswali haya:
Je, bado jina langu limeandikwa kwenye orodha ya wafuasi wa dini ya uwongo?
Je, ninashirikiana na shirika linalohusiana na dini nyingine?
Je, kazi yangu inaunga mkono dini ya uwongo kwa njia yoyote?
Je, kuna hatua nyingine ambayo ninahitaji kuchukua ili kujitenga na dini ya uwongo?
Ikiwa nimejibu ndiyo kwa mojawapo ya maswali hayo, ninapaswa kufanya mabadiliko gani?
Katika visa hivyo vyote, fanya uamuzi utakaokuacha ukiwa na dhamiri safi na utakaoonyesha kwamba wewe ni mshikamanifu kwa Yehova.
Utafanya nini ukiombwa utoe mchango wa kusaidia mashirika ya kidini?
WATU FULANI HUSEMA: “Ninahitaji kujua mambo ambayo waasi-imani wanasema kuhusu Mashahidi wa Yehova ili nitetee ukweli.”
-