-
Ole wa Pili—Majeshi ya Wapanda-FarasiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
6. Yohana anaelezaje habari ya majeshi ya wapanda-farasi anayofuata kuona?
6 “Na idadi ya majeshi ya wapanda-farasi ilikuwa mamiriadi mawili ya mamiriadi: mimi nilisikia idadi yao. Na hivi ndivyo mimi niliona wale farasi katika njozi, na walioketi juu yao: wao walikuwa na mabamba-kifua mekundu-moto na hayakintho-buluu na salfa-manjano; na vichwa vya farasi vilikuwa kama vichwa vya masimba, na katika vinywa vyao moto na moshi na salfa vilitoka. Kwa tauni tatu hizi theluthi ya wanadamu waliuawa, kwa moto na moshi na salfa ambavyo vilitoka katika vinywa vyao.”—Ufunuo 9:16-18, NW.
7, 8. (a) Majeshi ya wapanda-farasi hutoka kwa kishindo yakiwa chini ya mwelekezo wenye uongozi wa nani? (b) Ni katika njia zipi majeshi ya wapanda-farasi ni kama nzige walioyatangulia?
7 Kwa wazi, majeshi ya wapanda-farasi hawa huenda kwa kishindo chini ya mwelekezo wenye kuongoza wa malaika wanne. Lo! ni tamasha yenye kutia hofu kama nini! Wazia tendo-mwitikio lako kama wewe ungekuwa ndiwe shabaha ya shambulio kama hilo la majeshi ya wapanda-farasi! Mwonekano wao wenyewe ungepiga moyo wako kwa hofu. Ingawa hivyo, je! wewe umeona jinsi majeshi ya wapanda-farasi hawa wanavyofanana na nzige waliowatangulia? Nzige walikuwa kama farasi; katika majeshi ya wapanda-farasi kuna farasi. Kwa hiyo, vikosi vyote viwili vinahusika katika vita ya kitheokrasi. (Mithali 21:31) Nzige walikuwa na meno kama ya masimba; farasi wa majeshi ya wapanda-farasi wana vichwa kama vya masimba. Kwa hiyo, vikosi vyote viwili vinafungamanishwa na Simba wa kabila la Yuda mwenye ushujaa Yesu Kristo, ambaye ndiye Kiongozi, Kamanda, na Kielelezo wao.—Ufunuo 5:5, NW; Mithali 28:1.
8 Nzige na majeshi ya wapanda-farasi pamoja hushiriki katika kazi ya hukumu ya Yehova. Nzige waliibuka katika moshi ambao ulionya kimbele juu ya ole na moto wenye uharibifu kwa Jumuiya ya Wakristo; katika vinywa vya farasi mnatoka moto, moshi, na salfa. Nzige walikuwa na mabamba-kifua ya chuma, kuashiria kwamba mioyo yao ililindwa na kujitoa kusikopindika kwa ajili ya uadilifu; majeshi ya wapanda-farasi yalivaa mabamba-kifua yenye rangi nyekundu, buluu, na manjano, kurudisha moto, moshi, na salfa ya jumbe za hukumu zenye kuleta kifo zinazofoka katika vinywa vya farasi. (Linga Mwanzo 19:24, 28; Luka 17:29, 30.) Nzige walikuwa na mikia kama nge kwa ajili ya kutesa; farasi wana mikia kama manyoka kwa ajili ya kuua! Inaonekana kwamba kilichoanzwa na nzige chapasa kifuatiliwe na majeshi ya wapanda-farasi kwa mkazo mkubwa zaidi hadi utimilifu.
9. Majeshi ya wapanda-farasi hufananisha nini?
9 Kwa hiyo haya majeshi ya wapanda-farasi hufananisha nini? Kama vile jamii ya Yohana iliyopakwa mafuta ilivyoanza mbiu kama ya tarumbeta ya hukumu ya Yehova ya kisasi cha kimungu dhidi ya Jumuiya ya Wakristo, wakiwa na mamlaka ya ‘kuchoma kwa uchungu na kudhuru,’ ndivyo sisi tungetazamia kikundi icho hicho chenye uhai kitumiwe katika ‘kuua,’ yaani, katika kujulisha kwamba Jumuiya ya Wakristo pamoja na viongozi wa kidini wayo ni wafu kiroho kabisa kabisa, wakiwa wametupiliwa mbali na Yehova na wako tayari kwa ajili ya “tanuri ya moto” ya uharibifu wa milele. Kweli kweli, sehemu yote ya Babuloni Mkubwa lazima ipotelee mbali. (Ufunuo 9:5, 10; 18:2, 8; Mathayo 13:41-43, NW) Hata hivyo, kwa kutangulia uharibifu wayo, jamii ya Yohana inatumia “ule upanga wa roho, yaani, neno la Mungu,” katika kufichua hali kama ya kifo ya Jumuiya ya Wakristo. Malaika wanne na wapanda-farasi hutoa mwelekezo kwa huu uuaji wa kitamathali wa “theluthi ya wanadamu.” (Waefeso 6:17; Ufunuo 9:15, 18, NW) Hiyo huonyesha upangaji unaofaa wa kitengenezo na mwelekezo wa kitheokrasi chini ya uangalizi wa Bwana Yesu Kristo wakati kikosi cha watangazaji Ufalme kinapotoka kasi kushambulia piganoni.
Mamiriadi Mawili ya Mamiriadi
10. Ni katika maana gani kuna mamiriadi mawili ya mamiriadi ya majeshi ya wapanda-farasi?
10 Kunawezaje kuwa na mamiriadi mawili ya mamiriadi ya haya majeshi ya wapanda-farasi? Kihalisi miriadi moja ni 10,000. Kwa sababu hiyo, mamiriadi mawili ya mamiriadi yangekuwa milioni 200.a Kwa furaha, sasa kuna mamilioni ya watangazaji wa Ufalme, lakini hesabu yao ni kasoro sana ya mamia ya mamilioni! Ingawa hivyo, kumbuka maneno ya Musa kwenye Hesabu 10:36, NW: “Urudi, O Yehova kwenye mamiriadi ya maelfu ya Israeli.” (Linga Mwanzo 24:60.) Kihalisi, hiyo ingemaanisha, ‘Urudi kwenye makumi ya mamilioni ya Israeli.’ Hata hivyo, Israeli walikuwa hesabu yapata milioni mbili au tatu katika siku ya Musa. Basi, Musa alikuwa akisema nini? Hapana shaka yeye alikuwa akilini na wazo la kwamba Waisraeli wapaswa kuwa wasiohesabika kama “nyota za mbingu na kama chembe za mchanga ambazo ziko ufuoni mwa bahari,” badala ya kuhesabiwa. (Mwanzo 22:17; 1 Nyakati 27:23, NW) Hivyo, yeye alitumia neno la “miriadi” kuonyesha hesabu kubwa lakini isiyoonyeshwa waziwazi. Hivyo, The New English Bible hufasiri mstari huu hivi: “Pumzika, BWANA wa maelfu yasiyohesabika ya Israeli.” Hii inaafikiana na fasili ya pili ya neno la “miriadi” linalopatikana katika kamusi za Kigiriki na Kiebrania: “halaiki isiyohesabika,” “halaiki.”—The New Thayer’s Greek-English Lexicon of the New Testament; A Hebrew and English Lexicon of the Old Testament ya Gesenius, iliyotafsiriwa na Edward Robinson.
11. Ili jamii ya Yohana iwe mamiriadi hata katika maana ya ufananisho, ni jambo gani lingehitajiwa?
11 Hata hivyo, wale wa jamii ya Yohana ambao wangali wanabaki duniani hesabu yao ni chache zaidi ya 10,000—punde kuliko miriadi moja halisi. Wangewezaje kulinganishwa na maelfu yasiyohesabika ya majeshi ya wapanda-farasi? Ili wawe mamiriadi hata katika maana ya ufananisho, je! wasingehitaji kupata miimarisho? Hilo ndilo wamekuwa wakihitaji, na kwa fadhili zisizostahiliwa za Yehova, hilo ndilo wamepokea! Hiyo imetoka wapi?
12, 13. Ni matukio gani ya kihistoria kutoka 1918 mpaka 1935 yaliyoonyesha chanzo cha miimarisho?
12 Tangu 1918 hadi 1922 jamii ya Yohana ilianza kutolea binadamu wenye taabu taraja lenye furaha la kwamba “mamilioni wanaoishi sasa hawatakufa kamwe.” Katika 1923, pia ilifanywa ijulikane kwamba “kondoo” wa Mathayo 25:31-34 wangerithi uhai duniani chini ya Ufalme wa Mungu. Tumaini linalofanana na hilo lilitolewa katika kijitabu Freedom for the Peoples, kilichotolewa kwenye mkusanyiko wa kimataifa katika 1927. Katika miaka ya mapema ya 1930 jamii nyoofu ya Yehonadabu na wale ‘watu wanaolia na kuugua’ juu ya hali ya kiroho yenye kusikitisha ya Jumuiya ya Wakristo walionyeshwa kuwa ni wale wale kondoo walio na mataraja ya uhai wa kidunia. (Ezekieli 9:4; 2 Wafalme 10:15, 16) Likielekeza hao kwenye “majiji ya makimbilio” ya ki-siku-hizi, The Watchtower la Agosti 15, 1934, lilitaarifu hivi: “Wale wa jamii ya Yonadabu wamesikia mvumo wa tarumbeta ya Mungu na wametii onyo kwa kukimbilia tengenezo la Mungu na kushirikiana na watu wa Mungu, na ni lazima wakae humo.”—Hesabu 35:6, NW.
13 Katika 1935 wale wa jamii hii ya Yonadabu walialikwa kipekee wahudhurie mkusanyiko wa Mashahidi wa Yehova katika Washington, D.C. U.S.A. Huko, Ijumaa, Mei 31, J. F. Rutherford alitoa hotuba yake yenye kujulikana sana “Mkutano Mkubwa,” ambayo katika hiyo yeye alionyesha waziwazi kwamba kikundi hiki cha Ufunuo 7:9 kilikuwa ni kile kile kama wale “kondoo” wa Mathayo 25:33—kikundi kilicho wakfu chenye matumaini ya kidunia. Kama utangulizi wa mambo yatakayokuja, kwenye mkusanyiko huo Mashahidi wapya 840 walibatizwa, walio wengi wao wakiwa wa wale wa umati mkubwa.b
14. Je! umati mkubwa ungekuwa na sehemu katika shambulio la majeshi ya wapanda-farasi wa ufananisho, na ni azimio gani lililoonyeshwa katika 1963?
14 Je! huu umati mkubwa umekuwa na sehemu katika shambulio la majeshi ya wapanda-farasi lililoanza 1922 na ambalo lilipokea mkazo kwenye mkusanyiko wa Toronto katika 1927? Chini ya mwelekezo wa malaika wanne, jamii ya Yohana iliyopakwa mafuta, hakika wanayo. Kwenye mkusanyiko wenye kuzunguka ulimwengu “Habari Njema za Milele” mkusanyiko wa 1963, walijiunga na jamii ya Yohana katika azimio lenye kuamsha. Hilo lilijulisha wazi kwamba ulimwengu “wakabili tetemeko la dunia la matata ya ulimwengu kama ambalo haujapata kujua kamwe, na matengenezo yao yote ya kisiasa na Babuloni wa kidini wao yatatikiswa yawe vipande vipande.” Azimio lilitolewa kwamba “sisi tutaendelea kujulisha wazi watu wote bila upendeleo ‘habari njema za milele’ kuhusu ufalme wa Mungu wa Kimesiya na kuhusu hukumu zake, ambazo ni kama tauni kwa adui zake lakini ambazo zitatekelezwa kwa ajili ya ukombozi wa watu wote wanaotamani kuabudu Mungu Muumba kwa kukubalika, kwa roho na kwa ukweli.” Azimio hilo lilikubaliwa kwa idili katika makusanyiko 24 kuzunguka tufe lote na jumla ya wakusanyikaji 454,977, ambao zaidi ya asilimia 95 walikuwa wa ule umati mkubwa.
15. (a) Katika 2005 umati mkubwa ulijumlika kuwa asilimia gani ya kani-kazi ambayo Yehova anatumia shambani? (b) Ile sala ya Yesu kwenye Yohana 17:20, 21 inaonyeshaje umoja wao pamoja na jamii ya Yohana?
15 Umati mkubwa umeendelea kujulisha peupe umoja wao usio na masharti pamoja na ile jamii ya Yohana katika kumimina tauni juu ya Jumuiya ya Wakristo. Katika 2005 huu umati mkubwa ulijumlika kuwa asilimia 99.8 ya kani-kazi ambayo Yehova anatumia katika shamba. Washiriki wao wanapatana kabisa kabisa na jamii ya Yohana, ambao kwa habari yao Yesu alisali kwenye Yohana 17:20, 21, NW hivi: “Mimi nafanya ombi, si kuhusu hawa tu, bali pia kuhusu wale wanaoweka imani yao katika mimi kupitia neno lao; ili kwamba wote wapate kuwa mmoja, kama vile wewe, Baba, ulivyo katika muungano pamoja na mimi na mimi katika muungano pamoja na wewe, kwamba wao pia wapate kuwa katika muungano pamoja na sisi, ili kwamba ulimwengu upate kuitikadi kwamba wewe ulituma mimi niende.” Jamii ya Yohana inapoongoza ikiwa chini ya Yesu, umati mkubwa unashiriki pamoja nao katika shambulio la majeshi ya wapanda-farasi lenye mkumbo ulio mkubwa zaidi sana katika historia yote ya kibinadamu!c
-
-
Ole wa Pili—Majeshi ya Wapanda-FarasiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
a Commentary on Revelation, ya Henry Barclay Swete husema hivi kuhusu hesabu “mamiriadi mawili ya mamiriadi”: “Hesabu hizi kubwa mno hukataza sisi kutafuta utimizo halisi, na elezo linalofuata huunga mkono mkataa huu.”
-