-
Mashahidi wa YehovaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Pendekezo lingine: ‘Asante kwa kuuliza swali hilo. Tungependa kuona hali zikiwa bora, sivyo? Hebu nikuulize, Wewe unaonaje yale ambayo Yesu Kristo mwenyewe alifanya? Je, ungesema kwamba njia aliyotumia kuwasaidia watu ilikuwa nzuri? . . . Sisi hujaribu kufuata mfano wake.’
‘Wakristo wanapaswa kuwa mashahidi wa Yesu, wala si wa Yehova’
Unaweza kujibu hivi: ‘Hilo ni jambo lenye kupendeza. Na ni kweli kwamba tunapaswa kuwa mashahidi wa Yesu. Ndiyo sababu cheo cha Yesu katika kusudi la Mungu kinakaziwa katika vichapo vyetu. (Unaweza kutumia kitabu cha sasa au gazeti ili kuonyesha jambo hilo.) Lakini hapa pana jambo fulani ambalo huenda likawa jipya kwako. (Ufu. 1:5) . . . Yesu alikuwa “Shahidi Mwaminifu” wa nani? (Yoh. 5:43; 17:6) . . . Yesu alituwekea mfano tunaopaswa kufuata, sivyo? . . . Kwa nini ni muhimu sana kumjua Yesu na Baba yake pia? (Yoh. 17:3)’
-
-
MbinguKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Mbingu
Maana: Makao ya Yehova Mungu na viumbe roho waaminifu; makao yasiyoonekana kwa macho ya kibinadamu. Biblia pia inatumia neno “mbingu” katika maana nyingine mbalimbali; kwa mfano: kuwakilisha Mungu mwenyewe, tengenezo lake la viumbe roho waaminifu, hali ya kuwa na kibali cha Mungu, ulimwengu unaoonekana mbali na dunia, anga inayozunguka Dunia, serikali za kibinadamu chini ya utawala wa Shetani, na serikali mpya ya mbinguni yenye uadilifu ambayo Yesu Kristo pamoja na warithi-washirika wake wamepewa mamlaka na Yehova watawale ndani yake.
Je, sisi sote tulikuwa katika makao ya kiroho kabla hatujazaliwa tukiwa wanadamu?
Yoh. 8:23: “[Yesu Kristo alisema:] ‘Ninyi mnatoka kwenye makao ya chini; mimi ninatoka kwenye makao ya juu. Ninyi mnatoka katika ulimwengu huu; mimi sitoki katika ulimwengu huu.’” (Yesu alitoka katika makao ya kiroho. Lakini, kama Yesu alivyosema, wanadamu wengine hawakutoka huko.)
Rom. 9:10-12: “Rebeka alipochukua mimba ya mapacha . . . Walipokuwa bado hawajazaliwa wala kufanya jambo lolote jema au baya, ili kusudi la Mungu kuhusu kuchagua
-