Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ungamo
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Efe. 4:32: “Iweni wenye fadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma nyororo, mkisameheana kwa hiari kama vile Mungu pia kupitia Kristo alivyowasamehe ninyi kwa hiari.”

      Mtu anapofanya kosa zito na anataka kusaidiwa kiroho

      Yak. 5:14-16: “Je, kuna yeyote mgonjwa [kiroho] kati yenu? Na awaite kwake wanaume wazee wa kutaniko, nao wasali juu yake, wakimpaka mafuta katika jina la Yehova. Na sala ya imani itamponya huyo asiyejisikia vizuri, na Yehova atamwinua. Pia, ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa [na Mungu]. Kwa hiyo ungameni waziwazi dhambi zenu kwa mtu na mwenzake na kusali kwa ajili ya mtu na mwenzake, ili mponywe.”

      Met. 28:13: “Anayefunika makosa yake hatafanikiwa, lakini yeye anayeyaungama na kuyaacha ataonyeshwa rehema.”

      Namna gani ikiwa watu wanaofanya dhambi hawatafuti msaada?

      Gal. 6:1: “Akina ndugu, hata mtu akijikwaa katika kosa fulani kabla ya yeye kulijua, ninyi mlio na sifa za kustahili kiroho jaribuni kumrekebisha upya mtu huyo katika roho ya upole, huku kila mmoja wenu akiendelea kujiangalia, ili wewe pia usije ukajaribiwa.”

      1 Tim. 5:20: “Watu walio na mazoea ya kutenda dhambi uwakaripie mbele ya watazamaji [yaani, mbele ya wale ambao wao binafsi wanalijua jambo hilo], ili wengine pia waogope.”

      1 Kor. 5:11-13: “Lakini sasa ninawaandikia ninyi mwache kuchangamana katika ushirika pamoja na mtu yeyote anayeitwa ndugu ambaye ni mwasherati au mtu mwenye pupa au mwabudu-sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi, hata msile chakula pamoja na mtu wa namna hiyo. . . . ‘Ondoeni yule mtu mwovu kati yenu.’”

  • Uovu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Uovu

      Maana: Jambo ambalo ni baya sana kiadili. Mara nyingi humaanisha jambo linalodhuru, lenye nia mbovu, au lenye uvutano unaoharibu.

      Kwa nini kuna uovu mwingi sana?

      Mungu hapaswi kulaumiwa. Aliwapa wanadamu mwanzo mkamilifu, lakini wanadamu wamechagua kupuuza matakwa ya Mungu nao hujiamulia wenyewe yaliyo mema na yaliyo mabaya. (Kum. 32:4, 5; Mhu. 7:29; Mwa. 3:5, 6) Kwa kufanya hivyo, wanatawaliwa na viumbe waovu wenye nguvu kuliko wanadamu.—Efe. 6:11, 12.

      1 Yoh. 5:19: “Ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki