Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Toa Magazeti Katika Huduma
    Huduma ya Ufalme—2005 | Februari
    • Toa Magazeti Katika Huduma

      1 ‘Magazeti yenu yanapendeza, yanatia moyo, na ni ya wakati unaofaa.’ ‘Magazeti yenu ndiyo majarida yenye kutia moyo zaidi ambayo nimewahi kusoma.’ Maneno hayo yanaonyesha maoni ya wasomaji duniani kote kuhusu Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Magazeti yetu ni vifaa muhimu sana vya kuwahubiria “watu wa namna zote” habari njema.—1 Tim. 2:4.

      2 Mfanya biashara fulani aliachiwa gazeti la Amkeni! lililompendeza. Baadaye, alisoma gazeti la Mnara wa Mlinzi lililoambatana na gazeti hilo. Toleo hilo la Mnara wa Mlinzi lilikuwa na makala iliyomchochea kuchunguza fundisho la Utatu ambalo alikuwa ameamini kwa muda mrefu. Jambo hilo liliamsha upendezi wake. Alibatizwa miezi sita baadaye. Mtu mwingine alipokea magazeti hayo kwa ukawaida, lakini hakuyasoma. Kwa upande mwingine, mke wake aliwaepuka Mashahidi lakini alisoma magazeti ambayo mume wake aliachiwa. Aliguswa moyo na ahadi ya Biblia juu ya dunia paradiso ambayo itajaa watu waadilifu. Baada ya muda, yeye, mwanaye, na dadake wakawa watumishi wa Yehova.

      3 Toa Magazeti Yote Mawili: Kama mifano ambayo imetajwa inavyoonyesha, hatuwezi kujua ni nani watakaosoma magazeti yetu, na ni nini kitakachoamsha upendezi wao. (Mhu. 11:6) Kwa hiyo, kuna manufaa kutoa magazeti yote mawili, Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, hata ingawa kwa kawaida tutazungumzia gazeti moja tu tunapotoa magazeti hayo. Katika hali fulani, huenda ikafaa kumtolea mtu magazeti kadhaa tofauti-tofauti.

      4 Inafaa kutenga siku moja kila juma ili kushiriki katika huduma ya kutoa magazeti. Kwenye Kalenda ya Mwaka wa 2005 ya Mashahidi wa Yehova, kila Jumamosi imetengwa kuwa “Siku ya Magazeti.” Kwa kuwa hali za watu na za maeneo hutofautiana, huenda wengine wakatenga siku tofauti ya kutoa magazeti. Je, wewe unashiriki katika huduma ya kutoa magazeti kila juma?

      5 Jiwekee Mradi: Tutazingatia zaidi huduma ya kutoa magazeti ikiwa tutajiwekea mradi wa kuwaachia watu idadi fulani ya magazeti kila mwezi. Je, kuna watu unaowapelekea magazeti kwa ukawaida? Je, wewe huwatolea magazeti watu unaokutana nao unapohubiri? Je, unaweza kutoa magazeti unapohubiri barabarani, kwenye maeneo ya biashara, na sehemu za umma? Je, wewe hubeba magazeti unaposafiri, unaponunua vitu, au unapoenda kuwaona watu ambao umepanga kukutana nao? Tumia vizuri kila fursa kuwasaidia wengine wanufaike na magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!

      6 Huenda pia tukaazimia kuwatolea watu magazeti ya zamani tuliyo nayo. Hata kama matoleo fulani ya magazeti ni ya mwezi mmoja au zaidi iliyopita, bado habari zilizomo ni muhimu. Watolee watu wenye kupendezwa. Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yamekuwa ‘neno la wakati unaofaa.’ (Met. 25:11) Na tuyatumie kuwasaidia mamilioni ya watu kumjua na kumtumikia Yehova.

  • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
    Huduma ya Ufalme—2005 | Februari
    • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti

      Mnara wa Mlinzi Jan. 15

      “Sote tunatamani kuishi maisha bora pamoja na watoto wetu, lakini wengi huhisi kwamba hawana uwezo huo. Je, unafikiri tuna uwezo wa kuamua jinsi wakati wetu ujao utakavyokuwa? [Ngojea jibu.] Gazeti hili linaonyesha kwamba kulingana na Biblia tuna uwezo huo, kwa kuwa wakati wetu ujao unategemea maamuzi tunayofanya sasa.” Soma Kumbukumbu la Torati 30:19.

      Amkeni! Jan. 22

      “Tunapokuwa na matatizo ya afya, sisi sote huthamini daktari anayejali hisia zetu. Lakini, je, unafikiri wagonjwa wengi hujali hisia za daktari? [Ngojea jibu.] Gazeti hili linazungumzia matatizo ambayo madaktari hukabili na jinsi matibabu yatakavyokuwa wakati ujao.” Soma Isaya 33:24.

      Mnara wa Mlinzi Feb. 1

      Je, wewe hufadhaika unapoona kwamba watu wengi leo hutendewa jeuri na kukandamizwa? [Taja jambo ambalo limetukia karibuni linalojulikana katika eneo lenu, na ungojee jibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi Mungu anavyouona uhai wa mwanadamu. Linaeleza pia jinsi atakavyowakomboa wanadamu kutoka katika mateso yanayowapata leo.” Soma Zaburi 72:12-14.

      Amkeni! Feb. 8

      “Kuwa na mfadhaiko ni mojawapo ya matatizo makubwa tunayokabili leo. Sivyo? [Ngojea jibu.] Biblia ilitabiri kwa usahihi kwamba hali ingekuwa hivyo. [Soma 2 Timotheo 3:1.] Gazeti hili linatoa mapendekezo yanayoweza kukusaidia wewe na familia yako kukabiliana na mfadhaiko.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki