Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Unyenyekevu wa Yehova Unamaanisha Nini Kwetu?
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Novemba 1
    • Unyenyekevu wa Yehova Unamaanisha Nini Kwetu?

      DAUDI alipatwa na hali ngumu. Alidhulumiwa na Mfalme Sauli, baba-mkwe wake mwenye wivu. Sauli alijaribu kumuua Daudi kwa mkuki mara tatu, na kwa miaka mingi akamwinda daima, akimlazimisha awe mkimbizi. (1 Samweli 18:11; 19:10; 26:20) Hata hivyo, Yehova alikuwa pamoja na Daudi. Alimwokoa kutoka kwa Sauli na maadui wengine. Kwa hiyo, tunaweza kuelewa hisia za Daudi alipoimba: ‘Yehova ni mwamba wangu na ngome yangu na Mwokoaji wangu. Wewe Yehova utanipa ngao yako ya wokovu, na unyenyekevu wako ndio hunifanya niwe mkuu.’ (2 Samweli 22:2, 36) Daudi alipata ukuu wa kadiri fulani katika Israeli. Hivyo basi, unyenyekevu wa Yehova ulihusikaje?

      Biblia inaposema kwamba Yehova ni mnyenyekevu, haimaanishi kwamba amepungukiwa kwa njia yoyote, wala yeye yuko chini ya wengine. Bali, sifa hiyo nzuri inaonyesha kwamba yeye huwahurumia sana wanadamu ambao hujitahidi kwa unyoofu kupata kibali chake, naye huwaonyesha rehema. Kwenye Zaburi 113:6, 7 tunasoma: “[Yehova] anajishusha kutazama mbingu na dunia, akimwinua mtu wa hali ya chini kutoka kwenye mavumbi.” ‘Kujishusha’ kwake humaanisha kwamba “yeye huinama chini apate kuona” au “hujinyenyekeza ili atazame.” (Today’s English Version; Young’s Literal Translation of the Holy Bible) Hivyo, kutoka mbinguni Yehova mwenyewe ‘aliinama,’ au ‘kujinyenyekeza,’ ili amsikilize Daudi, mtu asiye mkamilifu lakini mnyenyekevu ambaye alitamani kumtumikia. Kwa hiyo, Daudi anatuhakikishia hivi: “Yehova yuko juu, hata hivyo yeye humwona mnyenyekevu.” (Zaburi 138:6) Yehova alishughulika na Daudi kwa rehema, subira, na huruma, na hilo lapaswa kutuchochea tujitahidi kufanya mapenzi yake.

      Ingawa Yehova ndiye Mwenye Enzi Kuu na ana cheo cha juu zaidi ulimwenguni, yeye yu tayari kushughulika na kila mmoja wetu. Hilo linatupa uhakika wa kwamba tunaweza kumtegemea hata katika hali ngumu zaidi. Hatupaswi kuogopa kwamba atatusahau. Kuhusiana na watu wake wa Israeli la kale, Yehova anatajwa kwa kufaa kuwa yule ‘ambaye aliwakumbuka walipokuwa katika hali ya chini: kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.’—Zaburi 136:23.

      Tukiwa watumishi wa Yehova wa siku hizi, tunaweza kupatwa na magumu kama Daudi. Huenda tukawa tunadhihakiwa na wale wasiomjua Mungu, au labda tunapambana na afya mbaya au tumefiwa. Hata hali yetu iweje, iwapo moyo wetu ni mnyoofu, tunaweza kumfikia Yehova katika sala, tukimsihi atuonyeshe rehema. Yehova ‘atainama’ kututazama na kusikiliza sala zetu. Mtunga-zaburi aliyeongozwa na roho ya Mungu aliandika: “Macho ya Yehova yanawaelekea waadilifu, na masikio yake yanakielekea kilio chao cha kuomba msaada.” (Zaburi 34:15) Tunaguswa moyo sana tunapofikiria sifa ya Yehova ya unyenyekevu yenye kupendeza.

      [Picha katika ukurasa wa 30]

      Yehova yu tayari kusikiliza sala zetu kama alivyosikiliza sala za Daudi

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Novemba 1
    • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

      Kutaniko la Kikristo huonaje ulafi?

      Neno la Mungu hushutumu ulevi na ulafi kuwa tabia zisizowafaa wale wanaomtumikia Mungu. Kwa hiyo, kutaniko la Kikristo humwona mlafi asiyetaka kubadilika kwa njia ileile linavyomwona mtu aliye na zoea la ulevi. Mlevi au mlafi hawezi kuwa mshiriki wa kutaniko la Kikristo.

      Methali 23:20, 21 inasema: “Usiwe kati ya watu wanaokunywa divai mno, kati ya watu wanaokula nyama kwa ulafi. Kwa maana mlevi na mlafi watakuwa maskini, na kusinzia kutamvika mtu nguo zilizopasuka.” Katika Kumbukumbu la Torati 21:20 tunasoma kuhusu mtu “mkaidi na mwasi,” ambaye kulingana na Sheria ya Musa alistahili kuuawa. Kulingana na mstari huo, mtu huyo mwasi na asiyetubu alikuwa “mlafi na mlevi.” Ni wazi kwamba katika Israeli la kale, ulafi ulionwa kuwa zoea lisilofaa kwa waliotaka kumtumikia Mungu.

      Hata hivyo, mlafi ni mtu wa aina gani, nayo Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo husema nini kuhusu ulafi? Mlafi ni mtu ambaye “sikuzote hula na kunywa kwa pupa.” Hivyo, ulafi ni aina ya pupa, nalo Neno la Mungu hutuambia kwamba “watu wenye pupa” ni kati ya wale ambao hawataurithi Ufalme wa Mungu. (1 Wakorintho 6:9, 10; Wafilipi 3:18, 19; 1 Petro 4:3) Kwa kuongezea, wakati mtume

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki